Menu

JE ALIEFUNGUA BAADHI YA MASIKU KWA DHARURA ATAPATA FADHLA KAMA ZA YULE ALIFUNGA RAMADHANI KAMILI?


Suali : 

Imekuja katika sahihi mbili katika Hadithi ya Abu hureira Radhi za Allah ziwe juu yake yakwamba Mtume MUHAMMAD ﷺ amesema : [Atakaefunga Ramadhan hali yakua ana imani na anatarajia malipo basi atasamehewa madhambi yake yaliyopita.] jee yule aliyefungua baadhi ya masiku katika ramadhan kwa sababu ya udhuru jee fadhla hii ataipata ? Au fadhla hii ni kwa yule aliefunga ramadhani kamili.

Jawabu :
Ama baada ya kumshukuru Mwenyezi Mungu na kumswalia Mtume Muhammad ﷺ.
Udhahiri wa Hadithi hii na ALLAH ni mjuzi zaidi ni kwamba fadhla hii inaenea hata kwa yule ambae hakufunga Ramadhani kamili .imekuja katika kitabu cha (Faidhul Qadiir) alipozungumzia hadithi hii ya :

 

مَنْ صَامَ رَمَضَانَ إِيمَانًا وَاحْتِسَابًا غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ]    رواه البخاري ومسلم]

 

[Atakaefunga Ramadhan hali yakua ana imani na anatarajia malipo basi atasamehewa madhambi yake yaliyopita] Anasema Karmaany "Na lau atawacha kufunga katika Ramadhani na nia yake ni kwamba lau sio udhuru uliompata angelifunga basi ataingia katika hukmu hii kama vile akiswali hali yakua amekaa kwa udhuru basi atapata thawabu ya mwenye kusimama". mwisho
Na ALLAH ni mjuzi zaidi.


*Chanzo: Fatawa za Sheikh Al Munajid

Imefasiriwa na Mahamd Fadhil El Shiraziy


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

8031804
TodayToday887
Highest 07-31-2026 : 9991
US
Guests 87

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a8d8c44a8d0f5662493501787661380
title_6a8d8c44a8d6f3200194171787661380
title_6a8d8c44a8dca20187393341787661380

NISHATI ZA OFISI

title_6a8d8c44a965c19702216811787661380
title_6a8d8c44a96b9749523271787661380
title_6a8d8c44a96ed5399657601787661380 Add content here

HUDUMA MPYA

: 2 + 9 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

Go to top
UongofuUongofu.com