Menu

RUHUSA YA KUKUSANYA SWALA KWA MGONJWA


 

 

Suala; Je mgonjwa alie lala kitandani anaruhusiwa kukusanya Swala na kupunguza?
Jawabu: Mtu akishikwa na ugonjwa na akawa hawezi kusimama kuswali, basi Sheria imemruhusu kuswali kwa kukaa, na ikiwa hawezi kukaa basi aswali kwa ubavu na akishindwa kuswali kwa ubavu basi anaswali kwa kuashiria rukuu na kusujudu na hii ni kwa hadithi ya Imraan bin Huswein asema nilikuwa na bawasili, nikamuliza Mtume ﷺ Kuhusu Swala akasema:

صل قائماً، فإن لم تستطع فقاعداً، فإن لم ‏تستطع فعلى جنب]   رواه الجماعة إلا مسلما] 

[Swali kwa kusimama ikiwa hutoweza basi swali kwa kukaa na ikiwa hutoweza swali kwa ubavu]   [Imepokewa na Jamaa ila Muslim]
Na amejuzisha Imam Ahmad kukusanya swala, sawa kwa kutanguliza au kuakhirisha kwa udhuru wa ugonjwa, kwa sababu ugonjwa uko na shida zaidi kuliko shida ya Mvua.
Na Amesema Imam Annawawiy "ni Huja ya nguvu," yaani Hoja ya Imamu Ahmad
Na imekuja katika kitabu cha Al-Mughniy cha Ibnu Qudaama "Na ugonjwa unao ruhusiwa kukusanya ni ule unao mpatia mtu shida na udhaifu ikwa ataswali kila swala kwa wakati wake"
Na kauli hii ndio inayo kwenda sambamba na sheria yetu kwa sababu shida huleta wepesi.
Ama kupunguza swala kwa kuswali adhuhuri na alasiri na Ishaa rakaa mbili hili halifai kwa sababu lingekuwa lafaa mtume angemruhusu huyu Swahaba Imraan Bin Huswein alipo muuliza pamoja na kuwa Mtume alimruhusu kuacha baadhi ya nguzo kama kusimama kwa ajili ya kumsahilishia na hili lakupunguza kama lafaa basi Mtume  ange mruhusu.


Na Allah ndie Mjuzi zaidi.


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6785498
TodayToday499
Highest 07-17-2025 : 4917
US
Guests 31

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68a98c24b0cf42966647381755941924
title_68a98c24b0de01300998931755941924
title_68a98c24b0ec4228282541755941924

NISHATI ZA OFISI

title_68a98c24b24f94856172211755941924
title_68a98c24b25ec20744091491755941924
title_68a98c24b26b89955552381755941924 Add content here

HUDUMA MPYA

: 5 + 5 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com