Menu

BUSTANI YA WATU WEMA


RIYADHU


وعن أَبي العباسِ سهل بنِ سعدٍ السَّاعِدِيِّ  رضي اللَّه عنه أَن رسولَ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم قال يَوْمَ خَيْبَرَ : « لأعْطِيَنَّ الرَّايَةَ غَداً رَجُلاً يَفْتَحُ اللَّه عَلَى يَدَيْهِ ، يُحبُّ اللَّه ورسُولَهُ ، وَيُحبُّهُ اللَّه وَرَسُولُهُ » فَبَاتَ النَّاسُ يَدُوكونَ لَيْلَتَهُمْ أَيُّهُمْ يُعْطَاهَا . فَلَمَّا أصبحَ النَّاسُ غَدَوْا عَلَى رسولِ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم : كُلُّهُمْ يَرجُو أَنْ يُعْطَاهَا ، فقال: « أَيْنَ عليُّ بنُ أَبي طالب ؟ » فَقيلَ : يا رسولَ اللَّه هُو يَشْتَكي عَيْنَيْه قال : « فَأَرْسِلُوا إِلَيْهِ » فَأُتِي بِهِ ، فَبَصقَ رسولُ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم في عيْنيْهِ ، وَدعا لَهُ ، فَبَرأَ حَتَّى كَأَنْ لَمْ يَكُنْ بِهِ وَجعٌ ، فأَعْطَاهُ الرَّايَةَ . فقال عليٌّ رضي اللَّه عنه : يا رسول اللَّه أُقاتِلُهمْ حَتَّى يَكُونُوا مِثْلَنَا ؟ فَقَالَ : « انْفُذْ عَلَى رِسلِكَ حَتَّى تَنْزِلَ بِسَاحتِهِمْ، ثُمَّ ادْعُهُمْ إِلَى الإِسْلامِ ، وَأَخْبرْهُمْ بِمَا يجِبُ مِنْ حقِّ اللَّه تَعَالَى فِيهِ ، فَواللَّه لأَنْ يَهْدِيَ اللَّه بِكَ رَجُلاً وَاحِداً خَيْرٌ لَكَ مِنْ حُمْرِ النَّعَمَ»    متفقٌ عليه


Kutoka kwa Abul-‘Abbaas Sahl bin Sa’d As-Saa’idiy (Radhi za Allah ziwe juu yake) ya kwamba Mtume ﷺ alisema siku  ya Khaybar: [Kesho nitampatia mtu bendera ambaye kwa mikono yake Mwenyezi Mungu atafungua (mji huu). Mtu huyo anampenda Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na Mwenyezi Mungu na Mtume anampenda.]  Watu wakakesha wakifikiria na kuzungumza juu ya nani atayepatiwa bendera hiyo. Kulipopambazuka watu wote walikwenda kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ kila mmoja anatarajia kuwa atapatiwa yeye jukumu hilo. Akasema (Mtume ﷺ): [Yuko wapi ‘Ali bin Abiy Twaalib?] Wakasema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu Yeye anaumwa macho.” Akasema Mtume wa Mwenyezi Mungu : [Mleteni kwangu.]  Akaletwa kwake, na Mtume  akampaka mate yake katika macho na kumwombea Mwenyezi Mungu . ‘Ali akapona kabisa na ugonjwa huo (wa macho) mpaka ikaonekana kama kwamba hakuwa na ugonjwa wowote na hapo akapatiwa bendera. ‘Ali (Radhi za Allah ziwe juu yake) akasema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Nipigane nao mpaka wawe kama sisi?”  Akasema Mtume : [Endelea kwenda kwa kasi yako ya kawaida mpaka ufike katika bonde lao na hapo muweke kambi yenu. Kisha waite katika Uislamu na uwajulishe habari kuhusu yanayo wajibika kwao juu ya haki ya Mwenyezi Mungu kwao. Naapa kwa jina la Mwenyezi Mungu! Mwenyezi Mungu akimuongoa mtu mmoja kupitia kwako ni bora kuliko kundi la ngamia wekundu.]     [Imepokewa na Muslim]


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

 

Visitors Counter

7668231
TodayToday7994
Highest 04-18-2026 : 16767
US
Guests 331

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_69f17f561ee3120139485681777434454
title_69f17f561ee819730250651777434454
title_69f17f561eebb19512209351777434454

NISHATI ZA OFISI

title_69f17f561f56311849669791777434454
title_69f17f561f5b32735054851777434454
title_69f17f561f60212845958481777434454 Add content here

HUDUMA MPYA

: 13 + 10 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com