Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


Suali: Ni nini Maana ya Mali ya biashara?


Jawabu: Mali ya biashara ni kila kilichoandaliwa kwa lengo la kuuzwa na kununuliwa ili mtu apate faida.

Na bidhaa za biashara zimekusanya vitu vyote vya sampuli zote za mali ambayo sio pesa zinazotumika kununulia vitu, kama vile magari, nguo, vitambaa, vyuma, mbao, na vyenginevyo vilivyoandaliwa kwa biashara.

Suali: Ni ipi Hukumu ya zaka ya Mali ya biashara.?


Jawabu: Hukmu ya zaka ya mali ya biashara ni lazima; kwa kauli ya Mwenyezi Mungu mtukufu:

 

أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا أَنفِقُوا مِن طَيِّبَاتِ مَا كَسَبْتُمْ وَمِمَّا أَخْرَجْنَا لَكُم مِّنَ الْأَرْضِ}    البقرة:267}

 

[Enyi mlioamini! Toeni katika vile vizuri mlivyovichuma, na katika vile tulivyokutoleeni katika ardhi] [Al-Baqarah: 267].

Jumla ya wanavyuoni wametaja kwamba makusudio ya aya hii ni: Zaka ya mali ya biashara, na kwa kauli ya Mwenyezi Mungu mtukufu:

 

 خُذْ مِنْ أَمْوَالِهِمْ صَدَقَةً}    التوبة:103}

 

[Chukua kutoka kwa mali zao sadaka]  [At-Tawbah: 103] ,

Na mali ya biashara ni katika mali zilizo dhahiri, basi Kwa ajili hii ikawajibika kutolewa zaka.


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7668198
TodayToday7961
Highest 04-18-2026 : 16767
US
Guests 286

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_69f17e8ac8f151097385931777434250
title_69f17e8ac8f6a12256999541777434250
title_69f17e8ac8fb916845359311777434250

NISHATI ZA OFISI

title_69f17e8ac990811098505241777434250
title_69f17e8ac996a19713829611777434250
title_69f17e8ac99c63800935941777434250 Add content here

HUDUMA MPYA

: 10 + 11 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com