Menu

SOMO LA FIQHI


 somo lafiqhi


Suali: Ni yapi masharti ya mtu kuwajibika kutoa zaka za mali ya biashara?

Jawabu: Masharti ya kulazimika mtu kutoa zaka ya Mali ya biashara.
1. Kiwango chake kifikie nisabu, na nisabu inakadiriwa kwa kipimo cha dhahabu na fedha.

2. Ikamilishe mzunguko wa mwaka mzima.

3. Iwe imekusudiwa kwa lengo la biashara; na hii ni kwamba iwe imekusudiwa kama kuchuma; kwa kauli ya Mtume:

 

إنما الأعمال بالنيات]    رواه البخاري ومسلم] 

 

[Hakika ya matendo ni kwa niya ya mtu]    [Imepokewa na Bukhari na Muslim.].

Mtu atakapobadilisha niya yake kutoka kwa biashara na kutumia bidhaa hizo basi hukatika hisabu ya mzunguko (mwaka), na akirudia niya ya biashara ataanza tena upya kuhisabu mzunguko mpya, ila akiwa amekusudia kufanya udanganyifu kwa lengo la kuondosha jukumu la kutoa zaka, basi hapa mzunguko haukatiki.

- Mfano: mtu anunue ardhi mwezi wa mfungo nne kwa nia ya kufanya biashara kisha alipofika shabani akageuza nia na akakusudia kujenga nyumba ya kukaa, hapa mwaka utakatika, kisha mfungo mosi akamua kuifanyia biashara mwaka wake utahisabiwa mfungo mosi ila kama alifanya hivyo kwa njia ya hila na kukimbia asitoe zaka basi mwaka hautakatika.

FAIDA

ZAKA YA RASLIMALI

Kinachotolewa zaka katika mali za biashara ni raslimali ambayo kwamba imekusudiwa kwa lengo la kununua na kuuza ili mtu apate faida, ama raslimali ambayo kwamba ni ya mali za kukaa hazizunguki katika biashara yaani si za kununuliwa ili ziuzwe, basi raslimali kama hii haihisabiwi wakati wa kuhisabu bidhaa za biashara wala haitolewi zaka, mfano wake ni kama makabati, na jokofu/firiji ambazo zinahifadhi bidhaa za kuuzwa, na magari yanayobeba bidhaa, na vyombo vya kubebea bidhaa, na mfano wake.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

8031728
TodayToday811
Highest 07-31-2026 : 9991
US
Guests 123

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a8d8172da5565871582781787658610
title_6a8d8172da5a719937806621787658610
title_6a8d8172da5f617304909941787658610

NISHATI ZA OFISI

title_6a8d8172dac3f12223216191787658610
title_6a8d8172dac8e567599841787658610
title_6a8d8172dacdb19638225351787658610 Add content here

HUDUMA MPYA

: 14 + 1 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

Go to top
UongofuUongofu.com