Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


NAMNA YA KUTAYAMAMU.

1. Aupige mchanga kwa mikono yake pigo moja.

2. Kisha aipulize kupunguza vumbi.

3. Kisha apanguse uso wake kwa hiyo mikono mara moja.

4. Kisha apanguse upande wa nje wa wa vitanga vya mikono. Apanguse sehemu ya nje ya kitanga cha mkono wa kulia kwa sehemu ya ndani ya kitanga cha mkono wa kushoto, kisha nje ya kitanga cha mkono wa kushoto kwa sehemu ya

Na dalili ya namna ya kutayamamu ni hadithi ya Ammar Radhi za Allah ziwe juu yake

 

أن النَّبِيَّ ﷺ ضَرَبَ بِكَفَّيْهِ الْأَرْضَ، وَنَفَخَ فِيهِمَا، ثُمَّ مَسَحَ بِهِمَا وَجْهَهُ وَكَفَّيْهِ]     متفق عليه]

 

[Kwamba Mtume ﷺ alipiga ardhi kwa vitanga vyake viwili vya mkono, akavipuliza kisha akapangusa uso wake na vitanga vyake kwavyo]      [Imepokewa na Bukhari na Muslim.].

FARADHI ZA KUTAYAMAMU.

1. Kutia nia.

2. Kupangusa uso.

3. Kupangusa vitanga vya mikono.

4. Kufuatanisha: aanze kupangusa uso kisha vitanga viwili vya mikono.

5. Kufuliliza: Apanguse mikono miwili baada ya kupangusa uso papo kwa papo.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6785142
TodayToday143
Highest 07-17-2025 : 4917
US
Guests 30

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68a952b9b751c6713458781755927225
title_68a952b9b760514911660261755927225
title_68a952b9b76f316474188071755927225

NISHATI ZA OFISI

title_68a952b9b8c8f15090971461755927225
title_68a952b9b8d7213283904381755927225
title_68a952b9b8e5b5790996361755927225 Add content here

HUDUMA MPYA

: 13 + 9 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com