Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


1.HUKMU YA UVINDU NA UMANJANO

Mwanamke akiona damu ya manjano au iliyochanganyika baina ya umanjano na weusi, au akaona umajimaji tu, huwa ni moja ya hali mbili:

A). Ima aione wakati wa hedhi au imeungana na hedhi kabla ya utwahara:

Katika hali hii itapewa hukumu ya hedhi, kwa hadithi ya Aishah Radhi za Allah ziwe juu yake kwamba wanawake walikuwa wakimtumia kibakuli ambacho ndani yake kuna pamba yenye dowa rangi ya manjano, na yeye akiwambia:

 

[انتظرن لا تعجلن حتى ترين القصة البيضاء]

 

[Ngojeni musifanye haraka mpaka muone paku leupe] akikusudia kwa hilo ndio kutwahirika na hedhi

B). Ima aione wakati wa twahara:

Katika hali hii huwa haizingatiwi kuwa ni kitu chochote, na haimpasi udhu wala kuoga, kwa hadithi ya Ummu Atiyyah kwamba alisema:

 

كُنَّا لا نَعُدُّ الْكُدْرَةَ وَالصُّفْرَةَ بَعْدَ الطُّهْرِ شَيْئًا]     رواه أبوداود]

 

[Hatukuwa tukiizingatia damu iliyochafuka au iliyo manjano baada ya kujitwahirisha kuwa ni chochote]    [Imepokewa na Abu Daud.].


2. HUKMU YA KUKATIKA KATIKA KWA HEDHI:

Mwanamke aonapo damu siku moja na kukatika siku moja na mfano wake, basi yeye ni mojawapo wa hali mbili

1. Hali hiyo iendelee na yeye kila wakati:
Basi hiyo ni damu ya istihadhah

2. Iwe yakatikakatika:
Kwa namna ya kwamba ikawa yamjia wakati mwingine na atwahirika wakati mwingine. Basi hukumu yake ni kama ifuatayo:

a. Kukatika damu kukipungua kwa siku moja, basi kipindi hiko kitahesabiwa kuwa ni katika kipindi cha hedhi.

b. Na akioona katika kipindi cha utwahara dalili za damu, kama kuona paku leupe, basi kipindi hiki ni cha utwahara, liwe ni dogo au kubwa, au liwe chini ya siku moja au zaidi.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6785164
TodayToday165
Highest 07-17-2025 : 4917
US
Guests 37

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68a9565d092b215979554071755928157
title_68a9565d0939d18931487851755928157
title_68a9565d0947e15810292811755928157

NISHATI ZA OFISI

title_68a9565d0aa0c13985204911755928157
title_68a9565d0aaf010287619781755928157
title_68a9565d0abd22110572871755928157 Add content here

HUDUMA MPYA

: 6 + 2 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com