Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


TunAkusudia kwa ibara (Muda wa hedhi) kile kipindi ambacho mwanamke hutumika yaani huwamo hedhini.

Kipindi hiki tunaweza kukigawa katika sehemu tatu,kama ifuatavyo:-

KIPINDI KIFUPI

Huu ndio muda wa chini kabisa wa kutoka damu ya hedhi hiki ni kipindi cha masaa ishirini na nne (24). Hii inaamaanisha kuwa mwanamke anaweza kuingia hedhini mchana na usiku wake tu, kisha damu ikakatika.

KIPINDI KIREFU

Huu ndio muda wa juu kabisa wa kutoka damu ya hedhi. Hiki ni kipindi cha siku kumi na tano (15), mchana na usiku.

KIPINDI CHA GHALIBU

Huu ndio muda wa ada na desturi kwa wanawake walio wengi, yaani wanawake wengi hutumika katika kipindi hiki. Huu ni muda wa siku sita au saba.

MUDA WA UTWAHARA

Muda wa chini wa twahara, yaani kipindi cha chini ambacho mwanamke anakuwa katika twahara ni siku kumi na tano (15).

Hakuna ukomo (limit) wa wingi wa twahara kwani inawezakana kabisa mwanamke asipate hedhi kwa muda wa mwaka, miaka miwili au miaka kadhaa na hili limethibiti kwa majaribio

Mwanamke atakapoiona damu chini ya kipindi kifupi cha hedhi yaani chini ya masaa ishirini na nne au aliiona damu baada ya kule kipindi kirefu cha hedhi, yaani baada ya siku kumi na tano, damu hii itazingatiwa kisheria kuwa ni damu ya ISTIHAADHA na sio damu ya hedhi.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6668174
TodayToday862
Highest 06-05-2025 : 6758
US
Guests 17

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6866bc9dcf9087453055451751563421
title_6866bc9dcf9f414635767091751563421
title_6866bc9dcfad819072834681751563421

NISHATI ZA OFISI

title_6866bc9dd10af17128838691751563421
title_6866bc9dd119a16157273671751563421
title_6866bc9dd127a9152883041751563421 Add content here

HUDUMA MPYA

: 13 + 9 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com