Menu

SOMO LA FIQHI


 somo lafiqhi


Kuoga kunakopendekezwa

1. KUOGA KWA AJILI YA SWALA YA IJUMAA

Kwa kauli ya Mtume :

 

من توضأ، فبها ونعمت، ومن تغسل فالغسل أفضل]    رواه أبوداود]

 

[Mwenye kutawadha kwa ajili ya kwenda Ijumaa, hilo ni jambo zuri, na mwenye kuoga, basi kuoga ni bora]    [Imepokewa na Abu Daud.]

2. KUOGA WAKATI WA KUHIRIMIA KWA AJILI YA UMRA NA HIJA.

Imepokewa kutoka kwa Zaid bin Thabit kwamba yeye alimuona Mtume :

 

تَجَرَّدَ لإِهلالِهِ وَاغتَسَلَ]   رواه الترمذي]

 

[Akijiondoa na nguo za kawaida kwa ibada ya Hija na akaoga]   [Imepokewa na Tirmidhi]

3. KUOGA BAADA YA KUOSHA MAITI.    

 

مَن غَسَّلَ مَيتًا فَلْيَغتَسِلْ]    رواه أحمد والترمذي]

 

Kwa neno la Mtume ﷺ: [Mwenye kuosha maiti aoge]     [Imepokewa na Ahmad na Attirmidhiy.]

4. KUOGA BAADA YA KILA TENDO LA NDOA.

Imepokewa na Abu Rafi'i radhi za Allah ziwe juu yake kwamba Mtume ﷺ:

 

طَافَ ذَاتَ يَوْمٍ عَلَى نِسَائِهِ يَغْتَسِلُ عِنْدَ هَذِهِ وَعِنْدَ هَذِهِ ، قَالَ قُلْتُ : لَهُ يَا رَسُولَ اللَّهِ أَلَا تَجْعَلُهُ غُسْلًا وَاحِدًا قَالَ :  هَذَا أَزْكَى وَأَطْيَبُ وَأَطْهَرُ     رواه أبوداود

 

[Siku moja aliwapitia wake zake, na alikuwa akioga baada ya kumaliza kwa huyu na kwa yule. Mpokeaji asema: (Nikamwambia”Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! usiuoge mara moja? Akasema ﷺ  [Hili ni safi zaidi, bora zaidi na twahara zaidi]         [Imepokewa na Abu Daud.]

 

MAKATAZO

1- kuchelewesha kuoga janaba mpaka utoke wakati wa Swala.

2- kwa mwanamke aliyetwahirika na hedhi kuacha Swala ya wajibu. Na lau atwahirika kabla ya kutoka wakati wa adhuhuri kwa kadiri ya rakaa moja, basi itampasa aoge na aswali adhuhuri. Mtume amesema:

 

من أدرك من الصبح ركعة قبل أن تطلع الشمس فقد أدرك الصبح ومن أدرك ركعة من العصر قبل أن تغرب الشمس فقد أدرك العصر]    رواه البخاري ومسلم]

 

[Mwenye kuwahi rakaa moja ya asubuhu kabla ya kuchomoza jua, basi amewahi Swala ya asubuhi. Na mwenye kuwahi rakaa moja ya alasiri kabla ya jua kuzama, basi amewahi Swala ya alasiri]  [Imepokewa na Bukhari na Muslim.].


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7668631
TodayToday296
Highest 04-18-2026 : 16767
US
Guests 769

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_69f18c7066d8d16317122271777437808
title_69f18c7066e0111007003811777437808
title_69f18c7066e637041642831777437808

NISHATI ZA OFISI

title_69f18c7067c984430112401777437808
title_69f18c7067cfa1844037401777437808
title_69f18c7067d5816884199811777437808 Add content here

HUDUMA MPYA

: 13 + 10 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com