Menu

SOMO LA FIQHI


 somo lafiqhi


Saumu ya Ramadhani ina nguzo mbili za msingi, ambazo kusihi kwa saumu kunazitegemea.

Nguzo ya kwanza: Ni kutia nia: nao ni kuazimia kufunga mwezi wa Ramadhani. Na nia mahala pake ni moyoni na sio lazima kwa ulimi. Na wala haikupokelewa kwa Mtume kuwa alikuwa akiitemka nia na vile vile haikupokelewa kwa Maswahaba wake watukufu.

Kwa neno lake Mtume ﷺ:

 

إِنَّما الأَعْمَالُ بالنِّيَّاتِ وإنَّما لكُلِّ امْرِىءٍ ما نَوَى ]     رواه البخاري ومسلم]

 

[Hakika kila jambo analolifanya (mwanadamu) ni kulingamana na nia yake, na hakika kila mtu atalipwa kulingana na alivyonuilia]        [Imepokewa na Bukhari na Muslim.]

Na kwa neno lake Mtume ﷺ:

 

من لم يبيت الصيام من الليل فلا صيام له]     رواه الترمذي] 

 

[Asiyeleta nia ya swaumu usiku, hana swaumu]. Imepokelewa na Tirmidhiy]

Na uwajibu huu wa kutia nia ni kwa upande wa saumu ya fardhi tu. Ama saumu za sunna, nia inatosha hata baada ya kuingia kwa mchana maadamu mtu hajatenda lo lote miongoni mwa yabatilishayo saumu.

 

عائشة رضي الله عنه : دخل علي رسول الله صلى الله عليه وسلم ذات يوم ، فقال : [هل عندكم شيء ؟ ]  قلنا : لا . قال :[ فإني صائم ] . رواه مسلم 

Imepokelewa kutoka kwa Bibi Aysha-Allah amuwiye radhi-kwamba Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie aliingia kwake siku moja na kuuliza: [Je, mna cho chote?] Nikamjibu: Hapana, akasema: [Basi hakika mimi nimefunga].      [Imepokewa na Muslim]

 

Nguzo ya pili: Nikujizuia na yote yenye kuharibu Saumu  tokea kuchomoza kwa alfajiri mpaka kuzama kwa jua, kwa ushahidi wa neno lake Allah Mtukufu:

 

وَكُلُوا وَاشْرَبُوا حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَكُمُ الْخَيْطُ الْأَبْيَضُ مِنَ الْخَيْطِ الْأَسْوَدِ مِنَ الْفَجْرِ ۖ ثُمَّ أَتِمُّوا الصِّيَامَ إِلَى اللَّيْلِ ۚ}    البقرة:187}

 

"Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa alfajiri katika weusi wa usiku. Kisha timizeni Saumu mpaka usiku.     [2:187]


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7887141
TodayToday274
Highest 05-20-2026 : 12580
US
Guests 38

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a3ba19217f9f9716123281782292882
title_6a3ba19217fef152536651782292882
title_6a3ba1921803c8770942591782292882

NISHATI ZA OFISI

title_6a3ba1921860811304562291782292882
title_6a3ba192186564912204341782292882
title_6a3ba192186a216808272111782292882 Add content here

HUDUMA MPYA

: 4 + 12 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com