Menu

SOMO LA FIQHI


 somo lafiqhi


Saumu ya Ramadhani ina nguzo mbili za msingi, ambazo kusihi kwa saumu kunazitegemea.

Nguzo ya kwanza: Ni kutia nia: nao ni kuazimia kufunga mwezi wa Ramadhani. Na nia mahala pake ni moyoni na sio lazima kwa ulimi. Na wala haikupokelewa kwa Mtume kuwa alikuwa akiitemka nia na vile vile haikupokelewa kwa Maswahaba wake watukufu.

Kwa neno lake Mtume ﷺ:

 

إِنَّما الأَعْمَالُ بالنِّيَّاتِ وإنَّما لكُلِّ امْرِىءٍ ما نَوَى ]     رواه البخاري ومسلم]

 

[Hakika kila jambo analolifanya (mwanadamu) ni kulingamana na nia yake, na hakika kila mtu atalipwa kulingana na alivyonuilia]        [Imepokewa na Bukhari na Muslim.]

Na kwa neno lake Mtume ﷺ:

 

من لم يبيت الصيام من الليل فلا صيام له]     رواه الترمذي] 

 

[Asiyeleta nia ya swaumu usiku, hana swaumu]. Imepokelewa na Tirmidhiy]

Na uwajibu huu wa kutia nia ni kwa upande wa saumu ya fardhi tu. Ama saumu za sunna, nia inatosha hata baada ya kuingia kwa mchana maadamu mtu hajatenda lo lote miongoni mwa yabatilishayo saumu.

 

عائشة رضي الله عنه : دخل علي رسول الله صلى الله عليه وسلم ذات يوم ، فقال : [هل عندكم شيء ؟ ]  قلنا : لا . قال :[ فإني صائم ] . رواه مسلم 

Imepokelewa kutoka kwa Bibi Aysha-Allah amuwiye radhi-kwamba Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie aliingia kwake siku moja na kuuliza: [Je, mna cho chote?] Nikamjibu: Hapana, akasema: [Basi hakika mimi nimefunga].      [Imepokewa na Muslim]

 

Nguzo ya pili: Nikujizuia na yote yenye kuharibu Saumu  tokea kuchomoza kwa alfajiri mpaka kuzama kwa jua, kwa ushahidi wa neno lake Allah Mtukufu:

 

وَكُلُوا وَاشْرَبُوا حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَكُمُ الْخَيْطُ الْأَبْيَضُ مِنَ الْخَيْطِ الْأَسْوَدِ مِنَ الْفَجْرِ ۖ ثُمَّ أَتِمُّوا الصِّيَامَ إِلَى اللَّيْلِ ۚ}    البقرة:187}

 

"Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa alfajiri katika weusi wa usiku. Kisha timizeni Saumu mpaka usiku.     [2:187]


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6785720
TodayToday721
Highest 07-17-2025 : 4917
US
Guests 11

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68a9bacd790a06266476741755953869
title_68a9bacd791a0902487921755953869
title_68a9bacd7928918311982831755953869

NISHATI ZA OFISI

title_68a9bacd7a87f12849983971755953869
title_68a9bacd7a9669810329391755953869
title_68a9bacd7aa4213087093881755953869 Add content here

HUDUMA MPYA

: 7 + 8 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com