Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


Mpangilio wa Matendo katika Siku ya Iddi
Sunna katika mipangilio ya siku ya idd ni kama inavo fuata:

1.Kutupa vijiwe.

2. Kuchinja.

3. Kunyoa au kupunguza.

4. Kufanya Twawafu.

5. Kufanya sai kwa mwenye sai,

Na lau atatanguliza moja katika mambo haya juu ya jengine yafaa na hakuna ubaya wowote, kwa sababu MtumeAliruhusu hilo, lau mtu atanyoa kwanza kisha akatupa mawe itasihi, na lau atachinja kwanza kisha akafanya Twawafu kisha akatupa vijiwe ni sawa, kwa sababu hakulizwa Mtume ﷺ kwa mwenye kutanguliza jambo na kuakhirisha jengine ila akisema:

 

افْعَلْ وَلاَ حَرَجَ]      متفق عليه]

 

[Fanya na hakuna ubaya]   [Imepokewa na Bukhari na Muslim.]

Kuhalalishiwa Mara ya Kwanza na Kuhalalishiwa Mara ya Pili:-

Kuhalalishiwa ya kwanza:

Ni kuhalalishiwa yote yale yalokuwa ni haramu kufanya kwa mwenye kuwa katika ihram isipokuwa kufanya tendo la ndoa au kufunga ndoa itakuwa si halali kwake kufanya hivyo, na inapatikana mtu kuhalalishiwa kwa kufanya mawili katika yanao fuata:

kutupa vijiwe kwenye jamaraat, kunyoa au kupunguza, kufanya Twawafu pamoja nakufanya sai kwa atake kuwa na sai

Kuhalalishiwa mara ya pili:

Ni kuhalalishiwa kufanya yote yale yaliokuwa ameharamishiwa kufanya alipokuwa kwenye ihram, na hupatikana uhalali wapili kwa kufanya yale yalio tangulia yote pamoja.

- Kuchinja haina mafungamano na kuhalalishiwa, lau atachelewesha kuchinja mpaka siku ya pili siku ya kumi na moja, na akafanya yale mengine siku ya idd atakuwa amehalalishwa.


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7887141
TodayToday274
Highest 05-20-2026 : 12580
US
Guests 38

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a3ba192608508832209471782292882
title_6a3ba192608a211271226071782292882
title_6a3ba192608ee17769718271782292882

NISHATI ZA OFISI

title_6a3ba19260f196490039211782292882
title_6a3ba19260f9620910390471782292882
title_6a3ba19260fe315825871471782292882 Add content here

HUDUMA MPYA

: 10 + 2 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com