Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


AINA ZA IBADA YA HIJA 

Aina za ibada ya Hija ni Aina Tatu:

1. Tamattu:
Nayo ni ahirimie Umra katika miezi ya Hijja mpaka amalize na ajitoe kwenye ihramu yake, kisha katika mwaka huohuo ahirimie Hija.

Na mwenye kufanya tamattu’ anapo fika makka atafanya amali ya Umra nayo: Nikutufu, na kufanya sai kati ya Swafaa na marwa, na kunyoa au kupunguza, kisha atajitoa kwenye ihramu yake na avae nguo zake, ikifika tarehe nane mwezi wa mfungotatu, atahirimia hija kisha atafanya amali za hijja na atawajibika kuchinja kwa kupumzika kwake

2. Qiraan:
Nayo ni ahirimie Hijja na Umra kwa pamoja., au ahirimie Umra kisha anuilie kufanya hija kabla ya kuanza kufanya tawafu, na mwenye kufanya Qiraan atabaki kwenye ihramu yake mpaka amalize kufanya hija, na atalazimika kuchinja kwa kule kuhirimia pamoja kwa amali ya hija na umra.

3. Ifraad:
Nayo ahirimie Hijja peke yake.na mwenye kufanya ifraadi atabaki na ihramu zake mpaka amalize kuhuji na hatolazimika kuchinja.

Na nusuk bora katika hizo tatu ni tamattu kwa sababu Mtume ﷺ Aliwaamrisha maswahaba zake wafanye tamattu  [Kwa hadithi iliyopokewa na Aisha Radhi za Allah ziwe juu yake iliyoko kwenye Sahihi ya Muslim.] Kisha ni Qiraan kisha ni Ifraad


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7668627
TodayToday292
Highest 04-18-2026 : 16767
US
Guests 652

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_69f18c2197b0d12545014291777437729
title_69f18c2197b7910118419261777437729
title_69f18c2197bda14512672011777437729

NISHATI ZA OFISI

title_69f18c219893320966149301777437729
title_69f18c21989946267528701777437729
title_69f18c21989f218789728311777437729 Add content here

HUDUMA MPYA

: 3 + 3 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com