Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


MAANA YA NUSUK

Nusuk Kilugha: Ni Ibada

Nusuk kisheria: Ni maneno yanayosemwa na vitendo vinavofanywa na Mwenye kuhiji au kufanya Umra.

NIA YA IBADA YA HIJJA (NUSUK)
Anapomaliza kuoga na kujinadhifisha yule anayetaka kuhirimia, akavaa nguo za ihramu, na mwanamume akatoa nguo za mzunguko, atanuilia kuingia kwenye ibada ya Hijja au Umra.

Na inapendekezwa aitamke aina ya ibada anayoikusudia. Aseme akikusudia Umra kisha kujistarehesha mpaka Hijja:

 

[لبيك اللهم عُمْرَة متمتعًا بها إلى الحج]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA UMRATAN MUTAMATIAN ILAA-L HAJJI

Nakuitikia, ewe Mola, kwa kufanya Umra hali ya kujipumzisha nayo mpaka nifanye ibada ya Hijja

au aseme:

[لبيك اللهم عُمْرَة]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA UMRATAN

Nakuitikia kwa kufanya Umra kisha wakati wa Hijja aseme:

 

[لبيك اللهم حجًّا]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA HAJJA

Nakuitikia kwa kuhiji. Na mwenye kuzishikanisha pamoja Hijja na Umra atasema:

 

[لبيك اللهم حجًّا وعُمْرَة]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA HAJJAN WA UMRAH

Nakuitikia kwa Hijja na Umra.

Kwa hadithi ya Anas Radhi za Allah ziwe juu yake  kuwa alisema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ akisema:

 

[لَبَّيْكَ عُمْرَةً وَحَجًّا]

 

[Nakuitikia Kwa kuhiji na kufanya Umra]   [Imepokewa na Bukhari na Muslim.].

Na asipotamka chochote nia ya moyoni inamtosheleza.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6785524
TodayToday525
Highest 07-17-2025 : 4917
US
Guests 27

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68a98fb749eac19585245311755942839
title_68a98fb749fa912203850161755942839
title_68a98fb74a09319110417461755942839

NISHATI ZA OFISI

title_68a98fb74d9605821471001755942839
title_68a98fb74da5c17044642991755942839
title_68a98fb74db3b13656295111755942839 Add content here

HUDUMA MPYA

: 13 + 4 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com