Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


MAANA YA NUSUK

Nusuk Kilugha: Ni Ibada

Nusuk kisheria: Ni maneno yanayosemwa na vitendo vinavofanywa na Mwenye kuhiji au kufanya Umra.

NIA YA IBADA YA HIJJA (NUSUK)
Anapomaliza kuoga na kujinadhifisha yule anayetaka kuhirimia, akavaa nguo za ihramu, na mwanamume akatoa nguo za mzunguko, atanuilia kuingia kwenye ibada ya Hijja au Umra.

Na inapendekezwa aitamke aina ya ibada anayoikusudia. Aseme akikusudia Umra kisha kujistarehesha mpaka Hijja:

 

[لبيك اللهم عُمْرَة متمتعًا بها إلى الحج]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA UMRATAN MUTAMATIAN ILAA-L HAJJI

Nakuitikia, ewe Mola, kwa kufanya Umra hali ya kujipumzisha nayo mpaka nifanye ibada ya Hijja

au aseme:

[لبيك اللهم عُمْرَة]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA UMRATAN

Nakuitikia kwa kufanya Umra kisha wakati wa Hijja aseme:

 

[لبيك اللهم حجًّا]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA HAJJA

Nakuitikia kwa kuhiji. Na mwenye kuzishikanisha pamoja Hijja na Umra atasema:

 

[لبيك اللهم حجًّا وعُمْرَة]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA HAJJAN WA UMRAH

Nakuitikia kwa Hijja na Umra.

Kwa hadithi ya Anas Radhi za Allah ziwe juu yake  kuwa alisema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ akisema:

 

[لَبَّيْكَ عُمْرَةً وَحَجًّا]

 

[Nakuitikia Kwa kuhiji na kufanya Umra]   [Imepokewa na Bukhari na Muslim.].

Na asipotamka chochote nia ya moyoni inamtosheleza.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7887147
TodayToday280
Highest 05-20-2026 : 12580
US
Guests 43

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a3ba2cc63bc34989452381782293196
title_6a3ba2cc63c1215461137951782293196
title_6a3ba2cc63c5e7022134081782293196

NISHATI ZA OFISI

title_6a3ba2cc6426310620466321782293196
title_6a3ba2cc642af10066418391782293196
title_6a3ba2cc642fa14514583761782293196 Add content here

HUDUMA MPYA

: 4 + 13 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com