Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


MAANA YA NUSUK

Nusuk Kilugha: Ni Ibada

Nusuk kisheria: Ni maneno yanayosemwa na vitendo vinavofanywa na Mwenye kuhiji au kufanya Umra.

NIA YA IBADA YA HIJJA (NUSUK)
Anapomaliza kuoga na kujinadhifisha yule anayetaka kuhirimia, akavaa nguo za ihramu, na mwanamume akatoa nguo za mzunguko, atanuilia kuingia kwenye ibada ya Hijja au Umra.

Na inapendekezwa aitamke aina ya ibada anayoikusudia. Aseme akikusudia Umra kisha kujistarehesha mpaka Hijja:

 

[لبيك اللهم عُمْرَة متمتعًا بها إلى الحج]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA UMRATAN MUTAMATIAN ILAA-L HAJJI

Nakuitikia, ewe Mola, kwa kufanya Umra hali ya kujipumzisha nayo mpaka nifanye ibada ya Hijja

au aseme:

[لبيك اللهم عُمْرَة]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA UMRATAN

Nakuitikia kwa kufanya Umra kisha wakati wa Hijja aseme:

 

[لبيك اللهم حجًّا]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA HAJJA

Nakuitikia kwa kuhiji. Na mwenye kuzishikanisha pamoja Hijja na Umra atasema:

 

[لبيك اللهم حجًّا وعُمْرَة]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA HAJJAN WA UMRAH

Nakuitikia kwa Hijja na Umra.

Kwa hadithi ya Anas Radhi za Allah ziwe juu yake  kuwa alisema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ akisema:

 

[لَبَّيْكَ عُمْرَةً وَحَجًّا]

 

[Nakuitikia Kwa kuhiji na kufanya Umra]   [Imepokewa na Bukhari na Muslim.].

Na asipotamka chochote nia ya moyoni inamtosheleza.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7887015
TodayToday148
Highest 05-20-2026 : 12580
US
Guests 75

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a3b805a8fd5818902233491782284378
title_6a3b805a8fdbd20970478391782284378
title_6a3b805a8fe0034984181782284378

NISHATI ZA OFISI

title_6a3b805aa58d515425044711782284378
title_6a3b805aa59277704444121782284378
title_6a3b805aa59731831376091782284378 Add content here

HUDUMA MPYA

: 12 + 11 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com