Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


MAANA YA NUSUK

Nusuk Kilugha: Ni Ibada

Nusuk kisheria: Ni maneno yanayosemwa na vitendo vinavofanywa na Mwenye kuhiji au kufanya Umra.

NIA YA IBADA YA HIJJA (NUSUK)
Anapomaliza kuoga na kujinadhifisha yule anayetaka kuhirimia, akavaa nguo za ihramu, na mwanamume akatoa nguo za mzunguko, atanuilia kuingia kwenye ibada ya Hijja au Umra.

Na inapendekezwa aitamke aina ya ibada anayoikusudia. Aseme akikusudia Umra kisha kujistarehesha mpaka Hijja:

 

[لبيك اللهم عُمْرَة متمتعًا بها إلى الحج]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA UMRATAN MUTAMATIAN ILAA-L HAJJI

Nakuitikia, ewe Mola, kwa kufanya Umra hali ya kujipumzisha nayo mpaka nifanye ibada ya Hijja

au aseme:

[لبيك اللهم عُمْرَة]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA UMRATAN

Nakuitikia kwa kufanya Umra kisha wakati wa Hijja aseme:

 

[لبيك اللهم حجًّا]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA HAJJA

Nakuitikia kwa kuhiji. Na mwenye kuzishikanisha pamoja Hijja na Umra atasema:

 

[لبيك اللهم حجًّا وعُمْرَة]

 

LABBAYKA ALLAHUMMA HAJJAN WA UMRAH

Nakuitikia kwa Hijja na Umra.

Kwa hadithi ya Anas Radhi za Allah ziwe juu yake  kuwa alisema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ akisema:

 

[لَبَّيْكَ عُمْرَةً وَحَجًّا]

 

[Nakuitikia Kwa kuhiji na kufanya Umra]   [Imepokewa na Bukhari na Muslim.].

Na asipotamka chochote nia ya moyoni inamtosheleza.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6668074
TodayToday762
Highest 06-05-2025 : 6758
US
Guests 25

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6866a3778ee468674162601751556983
title_6866a3778ef3121184169101751556983
title_6866a3778f0059522845301751556983

NISHATI ZA OFISI

title_6866a377903ed21126601691751556983
title_6866a377904c210678463481751556983
title_6866a377905971233859871751556983 Add content here

HUDUMA MPYA

: 14 + 10 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com