Menu

HUKMU YA KUSHEREHEKEA CHRISTMAS


Suali: Ndugu yetu anasema :anaona yakwamba baadhi ya Waislamu wanashirikiana na Wakristo katika sherehe za Christmas au sherehe za kuzaliwa Yesu kama wanavyoita na anaomba maelekezo.

Jawabu: Haifai kwa Muislamu wa kiume au wa kike kushirikiana na Manaswara au Mayahudi au wengine katika Makafiri katika sherehe zao, bali ni wajibu kuwacha hilo kwani,

[من تشبه بقوم فهو منهم]

 

[Atakaejifananisha na watu basi yeye ni katika wao]. Na Mtume Muhammad  ametutahadharisha kujifananisha na wasiokua Waislamu na kuiga tabia zao. Basi inampasa Muumini wa kike na wa kiume kujihadhari na jambo hilo na asisaidie kufanyika kwa sherehe hizi kwa jambo lolote, kwa sababu sherehe hizi ni sherehe ambazo ziko kinyume na sheria ya Mwenyezi Mungu, na wanaozisherehekea ni Maadui wa Mwenyezi Mung hivyo basi haifai kushiriki katika sherehe hizo wala kuwasaidia wenye kusherehekea kwa jambo lolote, sio kwa Chai wala Kahawa wala kwa jambo lolote kama vile vyombo na mfano wake.

Na pia Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

 

وَتَعَاوَنُوا عَلَى الْبِرِّ وَالتَّقْوَىٰ ۖ وَلَا تَعَاوَنُوا عَلَى الْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ}    المائدة:2}

 

[Na saidianeni katika wema na Ucha Mungu wala musisaidiane katika Maovu na Uadui]  [Al Maidah: 2.]
Hivyo basi kushirikiana na Makafiri katika sherehe zao ni sampuli ya kusaidiana katika Maovu na Uadui, ni wajibu kwa kila Muislamu kuwacha hilo la kusherehekea sherehe zisizokua za Kiislamu, na haifai kwa mwenye akili kughurika na watu katika matendo yao, la wajibu ni yeye kuangalia Sheria ya Kiislamu na iliyokuja katika Sheria, na afwate maamrisho ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake na asiangalie mambo ya watu kwani watu wengi hawajali Sheria za Mwenyezi Mungu kama alivyosema Mwenyezi Mungu katika kitabu chake kitukufu:

 

إِن تُطِعْ أَكْثَرَ مَن فِي الْأَرْضِ يُضِلُّوكَ عَن سَبِيلِ اللَّه}    الإنعام:116}

 

[Na ukiwat'ii wengi katika hawa waliomo Duniani watakupoteza na Njia ya Mwenyezi Mungu].  [Al An'aam: 116.]  Na anasema Mwenyezi Mungu alietukuka:

 

وَمَا أَكْثَرُ النَّاسِ وَلَوْ حَرَصْتَ بِمُؤْمِنِينَ}    يوسف:103}

 

[Na wengi wa watu si wenye kuamini hata ukijitahidi]      [ Yusuf: 103]

Mambo ya kukhalifu Sheria haifai kuyachukua hata kama Watu wanayafanya.

Na Muumini analinganisha Matedo yake na kauli zake na analinganisha matendo na kauli za watu na Qur'ani na Sunna zikiafikiana hiyo ndio yenye kukubaliwa hata kama wataiacha watu, na yakikhalifiana Maneno na matendo yake na Kitabu na Sunna basi hayatokubaliwa hata wakayafanya watu. Mwenyezi Mungu awaruzuku wote tawfiiq na uongofu.


*Chanzo: Fatawa ya Sheikh Ibnu Baaz

Imefasiriwa na Mahamd Fadhil El Shiraziy


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

8031725
TodayToday808
Highest 07-31-2026 : 9991
US
Guests 120

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a8d80c35fd775083786371787658435
title_6a8d80c35fdd8867672381787658435
title_6a8d80c35fe364772995301787658435

NISHATI ZA OFISI

title_6a8d80c3606456789394001787658435
title_6a8d80c3606a315818682271787658435
title_6a8d80c3606f218534500811787658435 Add content here

HUDUMA MPYA

: 9 + 13 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

Go to top
UongofuUongofu.com