Menu

HUKMU YA MWANAMKE WA KIISLAMU KUVAA WIGI KWA AJILI YA KUMPABIA MUMEWE


Suali?

Ni ipi hukmu ya mwanamke kuvaa (Mawigi) au nywele za kuvisha ili ajipambe kwa ajili ya mume wake ?
Jawabu :
Alhamdulillah , inatakiwa kwa Mume na Mke kijipamba kwa ajili ya mwenza wake kwa anacho kipenda, na atie nguvu mahusiano baina yao lakini katika mipaka yaliyohalalishwa na Sheria ya Kiislamu sio yaliyoharamishwa na sheria, na kuvaa Mawigi ilianza kuvaliwa na wanawake wasiokua Waislamu na wakajulikana kwa kuvaa mawigi na kujipamba nayo mpaka ikawa ni alama yao, hivyo basi Mwanamke kuvaa Wigi na kujipamba nayo hata kama ni kwa ajili ya Mume wake kuna kujifananisha na makafiri, na Mtume Muhammad amekataza jambo hilo kwa neno lake:

 

مَنْ تَشَبَّهَ بِقَوْمٍ فَهُوَ مِنْهُمْ]    رواه أبوداود]

 

[Atakaejifananisha na watu basi yeye ni miongoni mwao]   imepokewa na Abuu Dawud

na kwa sababu Wigi inaingia katika hukmu ya kuunganisha nywele bali ni mbaya zaidi kuliko kuunganisha nywele na Mtume amekataza jambo hilo na akamlaani mwenye kulifanya .
Fatwa za kamati ya kudumu ya fatwa 5/191.
Na amepokea Humeid bin Abdulrahman bin Auf yakwamba yeye amemsikia Muawiya bin Abi Sufyan (Radhi za Allah ziwe juu yao) mwaka wa Hijja na yeye akiwa juu ya Mimbar na yeye anasema na akachukua fungu la nywele ambalo lilikua katika mkono wa mlinzi wake wapo wana zuoni wenu nimemsikia Mtume rehma na amani ziwe juu yake akikataza jambo kama hili na anasema : kwa hakika waliangamia wana waisraeli pale wanawake wao walipojifanyia vitu hivi (yaani nywele za Kubandika).na imepokelewa kutoka kwa Abu Hureirah radhi za ALLAH ziwe juu yake kutoka kwa Mtume Muhammad ﷺ amesema:

 

لَعَنَ اللَّهُ الْوَاصِلَةَ وَالْمُسْتَوْصِلَةَ وَالْوَاشِمَةَ وَالْمُسْتَوْشِمَةَ]     رواه البخاري ومسلم]

 

[Mwenyezi Mungu amemlaani mwanamke mwenye kuunganisha nywele na mwenye kuunganishiwa na mwenye kuchora Tatoo na mwenye kuchorewa]  [imepokelewa na Bukhary na Muslim]

na ALLAH ndie mjuzi zaid


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7887143
TodayToday276
Highest 05-20-2026 : 12580
US
Guests 31

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a3ba2175ac9810503933661782293015
title_6a3ba2175ace918243696851782293015
title_6a3ba2175ad364200856591782293015

NISHATI ZA OFISI

title_6a3ba2175b2f911425526671782293015
title_6a3ba2175b3479345567381782293015
title_6a3ba2175b3958918701801782293015 Add content here

HUDUMA MPYA

: 10 + 11 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com