Menu

AR-RAHEEQ AL-MAKHTUM


Quresh


Baada ya uchunguzi inaonekana kuwa japokuwa mpaka wakati huo Da'awa ilikuwa bado ni ya siri, Makuraishi walikuwa wamekwisha kusikia khabari za Mtume na mafundisho yake, lakini wao walizipuuza khabari hizo. 

Muharnmad Al-Ghazali amesema, "Khabari hizi zilienea kwa Makuraishi, lakini wao hawakuzipa umuhimu wowote, na huenda walimdhani kuwa Muhammad ni mmoja wa hao watu ambao wanajihusisha na masuala ya dini, wanaozungumzia mambo ya Uungu na haki zake, kama alivyofanya Umayya bin Abi As-Salti na Quss bin Sa'idah, , Amru bin Nufail, na wengineo. Makuraishi walizinduka baada ya kipindi fulani kupita, walianza kupata khofu kwa jinsi ujumbe wake ulivyoenea kwa kasi na jinsi watu walivyokuwa wakiupokea na kuenea kwa athari yake, wakaanza kufuatilia safari zake na Da'wa yake kwa makini zaidi." (1)

Wito wa siri uliendelea kwa muda wa miaka mitatu, na katika kipindi hiki, liliibuka kundi la Waislamu ambalo lilisisitiza udugu na ushirikiano, kuueneza ujumbe na kumtia hima Mtume katika msimarno wake. Baada ya hapo ndio sasa ukashuka Wahyi uliomtaka Mjumbe wa Mwenyezi Mungu kuwatangazia Dini watu wake kwa kuwabainishia haki na batili pamoja na kuyahujumu rnasanarnu yao. *


1) Fiqlti Sira, Uk. 76.

* Ar Raheeq Al Makhtuum 123


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7668629
TodayToday294
Highest 04-18-2026 : 16767
US
Guests 745

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_69f18c621d5cd8969932051777437794
title_69f18c621d63c8903863161777437794
title_69f18c621d69d6365833931777437794

NISHATI ZA OFISI

title_69f18c621e46812364452441777437794
title_69f18c621e4cf1769459981777437794
title_69f18c621e52e16240406581777437794 Add content here

HUDUMA MPYA

: 10 + 5 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com