Menu

AR-RAHEEQ AL-MAKHTUM


Quresh


Baada ya uchunguzi inaonekana kuwa japokuwa mpaka wakati huo Da'awa ilikuwa bado ni ya siri, Makuraishi walikuwa wamekwisha kusikia khabari za Mtume na mafundisho yake, lakini wao walizipuuza khabari hizo. 

Muharnmad Al-Ghazali amesema, "Khabari hizi zilienea kwa Makuraishi, lakini wao hawakuzipa umuhimu wowote, na huenda walimdhani kuwa Muhammad ni mmoja wa hao watu ambao wanajihusisha na masuala ya dini, wanaozungumzia mambo ya Uungu na haki zake, kama alivyofanya Umayya bin Abi As-Salti na Quss bin Sa'idah, , Amru bin Nufail, na wengineo. Makuraishi walizinduka baada ya kipindi fulani kupita, walianza kupata khofu kwa jinsi ujumbe wake ulivyoenea kwa kasi na jinsi watu walivyokuwa wakiupokea na kuenea kwa athari yake, wakaanza kufuatilia safari zake na Da'wa yake kwa makini zaidi." (1)

Wito wa siri uliendelea kwa muda wa miaka mitatu, na katika kipindi hiki, liliibuka kundi la Waislamu ambalo lilisisitiza udugu na ushirikiano, kuueneza ujumbe na kumtia hima Mtume katika msimarno wake. Baada ya hapo ndio sasa ukashuka Wahyi uliomtaka Mjumbe wa Mwenyezi Mungu kuwatangazia Dini watu wake kwa kuwabainishia haki na batili pamoja na kuyahujumu rnasanarnu yao. *


1) Fiqlti Sira, Uk. 76.

* Ar Raheeq Al Makhtuum 123


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6785144
TodayToday145
Highest 07-17-2025 : 4917
US
Guests 33

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68a952b9b751c6713458781755927225
title_68a952b9b760514911660261755927225
title_68a952b9b76f316474188071755927225

NISHATI ZA OFISI

title_68a952b9b8c8f15090971461755927225
title_68a952b9b8d7213283904381755927225
title_68a952b9b8e5b5790996361755927225 Add content here

HUDUMA MPYA

: 7 + 2 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com