Menu

AR-RAHEEQ AL-MAKHTUM


637


Ibni Hajar anasema: 'Kukatika kwa Wahyi kulikuwa kumekusudiwa kumuandaa Mtume na kumuondoa khofu aliyokuwa nayo, na ili ipatikane shauku ya kurejea huo wahyi.(1)

Baada ya kuondoka kwa vivuli vya kuoteshwa na zikathibiti alama za uhakika na Mtume akajua kwa yakini kuwa amekuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu Aliye Mkuu na Mtukufu, na kuwa aliyemjia ni Mjumbe wa mbinguni aliyetumwa kumletea khabari kutoka kwa Mwenyezi Mungu . Ikawa kutazamia kwake kuja kwa Wahyi ni sababu ya kuongezeka yakini; na uvumilivu wake ni maandalizi ya Wahyi kurejea. Jibril alimjia kwa mara ya pili. Bukhari amepokea kutoka kwa Jabir bin Abdillahi, kuwa yeye alimsikia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu akizungurnzia kukatika kwa wahyi: "Wakati ninakuienda, ghafla nilisikia sa uti kutoka mbinguni nikanyanyua macho yangu na kutazama mbinguni, nikamwona Malaika ambaye alinijia kaiika pango la Hiraa amekaa juu ya kiti, katikati ya mbingu na ardhi, nikapiga magoti na kuporomoka mpaka kwenye ardhi, niliposimama nikarudi nyumbani ninatetemeka. Nikisema, 'Nifunikeni, Nifunikeni, wakanifunika, na hapo Mwenyezi Mungu ﷺ Akateremsha Sura:

 

{يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ  قُمْ فَأَنذِرْ  وَرَبَّكَ فَكَبِّرْ  وَثِيَابَكَ فَطَهِّرْ  وَالرُّجْزَ فَاهْجُرْ}

 

[Ewe Uliyejifunika maguo. Simama uonye (viumbe). Na Mola wako umtukuze. Na nguo zako uzisafishe. Na mabaya yapuuze.]       [Al-Muddaththir:1-5]

kisha Wahyi ukawa unakuja kwa nguvu,' mfululizo na 
kufuatana.(2) *


1) Fathul Bari, Juzuu 1, Uk. 27.
2) Sahihil Bukhari, Kitab Ttafsir, Babu Rrijz Fahjur, [uzuu 2, Uk. 733.]

*Arraheeq Al Makhtum 108


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6668026
TodayToday714
Highest 06-05-2025 : 6758
US
Guests 14

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68669867761436184925161751554151
title_686698677622d16483867111751554151
title_686698677630d11008458791751554151

NISHATI ZA OFISI

title_68669867778e020131186481751554151
title_68669867779c8539681181751554151
title_6866986777aa45221158701751554151 Add content here

HUDUMA MPYA

: 13 + 9 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com