Menu

SAFARI YA KWENDA SHAM KWA AJILI YA BIASHARA


إلى أين كانت رحلة الشتاء والصيف


Alipofikisha umri wa miaka ishirini na tano, alitoka kuelekea Sham kwa madhumuni ya kufanya biashara katika mali ya Bi Khadija (r.a). Ibn Ishaq anasema: 'Bi khadija binti Khuwaylid alikuwa ni mwanamke mfanyabiashara mtukufu, aliyekuwa na mali nyingi, alikuwa akiwakodisha wanaume kutoka katika mali yake, alikuwa akiwapa mali yake waifanyie biashara kwa kuwapa kitu kutoka katika faida itakayopatikana. Shughuli kubwa za Makuraishi wakati huo ilikuwa ni kufanya biashara.


Bi Khadija alipopata khabari za Mjumbe wa Mwenyezi Mungu , kuhusu tabia ya ukweli katika mazungumzo yake, wingi wa uaminifu wake na ubora wa tabia zake,alipeleka ujumbe kwake akimuomba atoke na mali yake kuelekea Syria kwa madhumuni ya kufanya biashara na kwamba atampa malipo bora kabisa zaidi ya vile anavyofanya kwa wafanya biashara wengine. Mjumbe wa Mwenyezi Mungu alilikubali wazo hilo, akatoka na mali za Bi Khadija kuelekea Syria, akifuatana na kijana wake Bi Khadija aitwae Maysara.(1)


1) Ibnu Hisham, Juzuu 1, Uk. 187-188

Ar-raheeq Al Makhtum. 92


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

8031730
TodayToday813
Highest 07-31-2026 : 9991
US
Guests 120

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a8d81f6db1309049930321787658742
title_6a8d81f6db18019810165041787658742
title_6a8d81f6db1cc5134414861787658742

NISHATI ZA OFISI

title_6a8d81f6db81519203392481787658742
title_6a8d81f6db8683043748211787658742
title_6a8d81f6db8c11199049881787658742 Add content here

HUDUMA MPYA

: 4 + 2 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

Go to top
UongofuUongofu.com