Menu

 HUKMU YA KUTUMIA MAJI YALIO TUMIWA


 

Swali: Je yafaa mtu kutumia maji yalio tumiwa kujitwayarisha kukamilishia Udhu wake. Mfano; mtu akayakusanya maji ya kutawadhia kwenye chombo kisha maji

yale akayatumia katika kuoshea miguu je yafaa kufanya hivyo?

Jibu: kutumia maji yaliotumika katika twahara ni katika Mas'ala wanchuoni walio ikhtilalifiana  sawa au si sawa katika kuyatumia maji yale kukamilisha Udhu au kutawadhia upya.

Madh'habu ya Imamu Malik anaona yafaa kutumia kwa sababu maji yale ni twahara na waweza kutwahirishia ikiwa maji yale hayakubadilika lakini ni Makruhu kutumia.

Na msimamo huu ndio msimamo wa Sheikhul islam Ibn Taimiyah. Asema kwa sababu maji yalio tumika katika kuondoshea hadathi yamebaki katika utwahara wake,na imesihi

kutoka kwa Mtume ﷺ Akisema:

إن الماء طهور لا يُنجِّسُه شيء]   رواه أبو داود ، والترمذي]

 

[Hakika ya Maji ni Twahara hayanajisiki kwa kitu chochote]     [Imepokewa na Abuu

Dawud na Attirmidhiy] 

Maji hayawezi kuwa na janaba,wala hayawezi kuchukuwa hukmu ya janaba.

Lakini msimamo wa wengi katika wanachuoni wanaona maji yalio tumiwa hayafai kuyatumia katika kuondoshea hadathi. sawa iwe ni hadathi ndogo kama kutawadhia, au Hadathi kubwa, kama kuoga janaba na msimamo huu ndio msimamo wa wengi na ni katika kujiondoa kwenye shaka na khilafu.

Kwa hivyo itakuwa ni bora kutumia maji ambao hajatumiwa katika kuondoshea hadathi sawa kukamilishia Udhu au kutawadhia.

Na allah ndie Mjuzi zaidi.


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6668034
TodayToday722
Highest 06-05-2025 : 6758
US
Guests 21

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68669867761436184925161751554151
title_686698677622d16483867111751554151
title_686698677630d11008458791751554151

NISHATI ZA OFISI

title_68669867778e020131186481751554151
title_68669867779c8539681181751554151
title_6866986777aa45221158701751554151 Add content here

HUDUMA MPYA

: 12 + 14 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com