Menu

NI MASHATRI GANI YA MTU KULAZIMIKA KUFUNGA?


Suali: Ni yapi Mashrti ya mtu kuwajibika Kufunga Mwezi wa Ramadhani ?

Jawabu: Masharti ya mtu kuwajibika Kufunga ni kama ifuatavyo:
1. Uislamu: Haimlazimu kafiri kufunga,na hata kama atafunga saumu yako haikubaliwi,na vile ile aliye ritadi amali zake hazukubaliwi,kwa neno lake Mwenyezi Mungu aliyetukuka:

 

لَئِنْ أَشْرَكْتَ لَيَحْبَطَنَّ عَمَلُكَ وَلَتَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِين}    الزمر:65}

 

"Bila ya shaka ukimshirikisha Mwenyezi Mungu a'mali zako zitaanguka, na lazima utakuwa miongoni mwa wenye kukhasiri."      [Al-Zzumar:65]

kwa sababu Uislamu ni Shari ya kukubaliwa amali ya Mwanadamu.

2. Kubaleghe: Sio lazima kwa mtoto mdogo kufunga, lakini huamrishwa kufunga akiwa anaweza ili kumpa mazoezi ya saumu naye azoee.Kwa neno lake Mtume :

 

رفع القلم عن ثلاثة: الصبي حتى يحتلم والنائم حتى يستيقظ والمجنون حتى يفيق.]     أخرجه أحمد وأبو داود]

 

[Kalamu imeinuliwa juu ya watu watatu,Mtoto mpaka abaleghe,na alielala mpaka aamke,na Mwenda wazimu mpaka apoe]    [Imepokelewa na Ahmad na Abuu Daud]

3. Kuwa na akili: Sio wajibu kwa mwendawazimu kufunga.Kwa hadithi iliyo tangulia

4. Uwezo wa kufunga: Sio wajibu kufunga kwa mtu ambaye hawezi kufunga (labda amekuwa mzee sana ama afya yake haimruhusu kuhimili saumu).Kwa neno lake Mwenyezi Mungu aliyetukuka:

 

وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ}      البقرة:184}

 

"Na wale wasio weza, watoe fidiya kwa kumlisha masikini."      [Al-Baqara:184]

5. Kwa Mwanamke asiwe kuwa kwenye ada yake ya Mwezi, au damu yanifasi.ama akiwa katika ada yake ya mwezi au akiwa katika nifasi ni haramu kufunga na watalizimika kula na kulipa wakati mwengine kwa neno lake Bibi Aisha radhi za Allah ziwe juu yake asema:

 

كنا نحيض على عهد رسول الله صلى الله عليه وسلم فنؤمر بقضاء الصيام ولا نؤمر بقضاء الصلاة]   رواه أبوداود]

 

[Tulikuwa tukiingia kwenye hedhi zama za Mtume  tukiamrishwa kulipa Saumu wala hatuamrishwi kulipa Swala]    [Imepokewa na Abuu Daud]


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

8031727
TodayToday810
Highest 07-31-2026 : 9991
US
Guests 134

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a8d8165302a61497428651787658597
title_6a8d8165302f816656390241787658597
title_6a8d81653034517599344371787658597

NISHATI ZA OFISI

title_6a8d81653098b12209713941787658597
title_6a8d8165309d912857832701787658597
title_6a8d816530a2619526223681787658597 Add content here

HUDUMA MPYA

: 11 + 6 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

Go to top
UongofuUongofu.com