Menu

MAANA YA TAWHIDI NA UMUHIMU WAKE


التوحيد 1 1


Ni nini Maana ya Tawhidi:

Tawhidi ni kumpwekesha Menyezi Mungu katika Ibaada, Kumuabudu yeye peke yake, bila ya Kumshirikisha na kitu Chochote.
Na hili ndilo lengo alilo Umbiwa Mwanadamu katika huu ulimwengu kumuabudu Mwenyezi mungu na kumtii yeye peke yake.
Menyezi Mungu Anasema :

وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ}    الذريات:56}

 

[Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi]     [Al-Dhariyaat:56]

 

UMUHIMU WA TAWHIDI 

 

Tawhidi ni jambo bora sana,na kwa sababu hii Mwenyezu Mungu (SW) Ameshuhudia kwa nafsi yake na vile vile Malika Wameshudia,na pia walio pewa Ilimu,kuwa ALLA (S.W) ni moja na die anaefaa Kuabudiwa peke yake bila ya kushirikiswa na kitu Chochote.

Mwenyezi Mungu Anasema:

 


شَهِدَ اللَّهُ أَنَّهُ لَا إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ وَالْمَلَائِكَةُ وَأُولُو الْعِلْمِ قَائِمًا بِالْقِسْطِ ۚ لَا إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ}      آل عمران:18} 

 

[Mwenyezi Mungu, na Malaika, na wenye ilimu, wameshuhudia kuwa hakika hapana mungu ila Yeye, ndiye Mwenye kusimamisha uadilifu; hapana mungu ila Yeye Mwenye nguvu na Mwenye hikima]        [Al-Imraan:18

1. Miongoni mwa Umuhimu wa Tawhidi ni kuwa Manabii wote walikuja kulingani Watu wao Tawhidi Kumpwekesha Mwenyezi Mungu S.W  Mwenyezi Mungu Anasema:

 

وَلَقَدْ بَعَثْنَا فِي كُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولًا أَنِ اعْبُدُوا اللَّهَ وَاجْتَنِبُوا الطَّاغُوتَ}      النحل:36} 

 

[Na bila ya shaka tulimpeleka mtume katika kila ummah ya kwamba : Muabuduni Mwenyezi Mungu na muapukeni muovu (Shetwani)  ]    [ An-Nahl: 36]

2. Mtume ﷺ: Alipo kuwa akituma Maswahaba kwenda Kulingania sehemu Fulani kwanza alikuwa akiwausia kulingania watu katika Tawhidi yaani Kumpwekesha Mwenyezi Mungu (S.A) .

3.Mwenye kushikamana na Tawhidi husamehewa madhambi yake,na huepushwa na kukaa Motoni milele ,kinyume na Mwenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu,hatopata Msamaha wa Mola wake, Mwenyezi Mungu Anasema:

 

إِنَّ اللَّهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ ۚ}   النساء:48} 

 

[Hakika Mwenyezi Mungu hasamehe kushirikishwa na husamehe yasiyokuwa hayo kwa amtakae ] [Al-nnisaa: 48]

4.Mwenye kushikamana na Tawhidi huwa karibu zaidi na Mwenyezi Mungu,na pia hupata amani kamili na uongofu hapa Duniani na kesho Akhera.

 

الَّذِينَ آمَنُوا وَلَمْ يَلْبِسُوا إِيمَانَهُم بِظُلْمٍ أُولَٰئِكَ لَهُمُ الْأَمْنُ وَهُم مُّهْتَدُونَ}      الأنعام:82}

 

[Wale ambao wameamini na hawakuchanganya imani zao na dhulma watapata amani na wataongoka ]    [ Al-an'aam : 82]


SIKILIZA MADA HII NA SHEIKH SALIM KHATIB



LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7887004
TodayToday137
Highest 05-20-2026 : 12580
US
Guests 52

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a3b7ea8e92fe4845612601782283944
title_6a3b7ea8e934e18771017301782283944
title_6a3b7ea8e939917167132461782283944

NISHATI ZA OFISI

title_6a3b7ea8e993b13129557071782283944
title_6a3b7ea8e99888848013001782283944
title_6a3b7ea8e99d319542074241782283944 Add content here

HUDUMA MPYA

: 12 + 13 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com