Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


HIKMA YA KUTOA ZAKA YA FITRI.

1. Kumsafisha aliyefunga kutokana na mambo ya upuzi na uchafu, kama ilivyopokewa kutoka kwa Ibn Abbas asema:

فرض رسول الله صلى الله عليه وسلم زكاة الفطر طهرة للصائم من اللغو والرفث، وطعمة للمساكين]    رواه أبوداود]

 

[Amefaradhisha Mtume ﷺ Zaka ya Fitri kwa aliyefunga ili kumsafisha kutokana na upuzi na uchafu na ni chakula cha masikini]    [Imepokewa na Abu Daud.].

Na hii ni kwamba aliyefunga mara nyingi haepukani na michezo, na maneno ya upuzi, na mambo yasiyo na faida katika maneno, basi ikawa hii Zaka inamsafisha aliyefunga kwa aliyoyafanya katika matamshi haya yaliyoharamishwa, au yaliyochukizwa kufanywa, ambayo kwamba yanapunguza thawabu za matendo, na kuharibu saumu.

2. Masikini na mafakiri kupata nafasi nzuri ya kimahitaji siku ya Idd ili kuepukana na kuomba ambako kuna udhalilifu na unyonge siku ya Idd, jambo hili (Zaka fitri) litawafanya wawe na furaha na bashasha, ili washirikiane na watu wengine katika kufurahia Idd.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7887141
TodayToday274
Highest 05-20-2026 : 12580
US
Guests 38

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a3ba1da3a7cb5331274341782292954
title_6a3ba1da3a81a10157804661782292954
title_6a3ba1da3a88819832772301782292954

NISHATI ZA OFISI

title_6a3ba1da3ae6318889762981782292954
title_6a3ba1da3aeb16858741591782292954
title_6a3ba1da3aefd343700311782292954 Add content here

HUDUMA MPYA

: 9 + 13 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com