Menu

SOMO LA FIQHI


 somo lafiqhi


Ili upangusaji juu ya khofu usihi kisheria ni lazima yapatikane sharti kadhaa kama zilivyotajwa na Wanachuoni. Miongoni mwa sharti muhimu kabisa ni hizi zifuatazo:-

1.Kuzivaa baada kujitwahirisha kikamilifu.

Kwa Hadithi iliopokelewa na Al Mughirah Radhi za Allah zawe juu yake asema:

 

كُنْتُ مَعَ النَّبِيِّ فِي سَفَرٍ فَأَهْوَيْتُ لِأَنْزِعَ خُفَّيْهِ، فَقَال: دَعْهُمَا، فَإِنِّي أَدْخَلْتُهُمَا طَاهِرَتَيْنِ. فَمَسَحَ عَلَيْهِمَا]     متفق عليه]

 

[Nilikuwa na Mtume safarini, nikaporomoka ili kuzivua khofu zake, akasema: [Ziache, kwani mimi nimezivaa katika hali ya utwahara  akapukusa juu yake]   [Imepokewa na Bukhari na Muslim.]

2. Ziwe ni zenye kusitiri miguu mpaka kwenye vifundo

zikiwa hazikusitiri Miguu mpaka kwenye vifundo viwili haifai kupangusa juu ya khofu hizo.

3. Ziwe zimetengezwa kwa vitu vilivyo twahara.

Ikiwa khofu zimetengenezwa kwa vitu vya Najisi basi haifai kupangusa juu yake.

4. Ziwe zinafaa kutumiwa na zisiwe ni miongoni mwa vitu haramu kama hariri kwa wanaume.

5. Kule kupukusa kuwe ndani ya muda uliowekwa. Kwani Mtum ﷺ aliweka muda maalumu wa kupukusa usiku na mcha kwa mkazi na siku tatu kwa msafiri. Haifai kupitisha muda huo.

6. Kupukusa kuwe kwenye kujitwahirisha kutokana twahara ndogo, kama kutangukiwa na udhu na sio tukio kubwa la ukosefu wa twahara. Imepokewa na Swafwan bin Assal Radhi za Allah ziwe juu yake kuwa alisema: 

 

كَانَ رَسُولُ اللهِ  يَأْمُرُنَا إِذَا كُنَّا مُسَافِرِينَ أَنْ نَمْسَحَ عَلَى خِفَافِنَا، وَلَا نَنْزِعَهَا ثَلَاثَةَ أَيَّامٍ مِنْ غَائِطٍ، وَبَوْلٍ، وَنَوْمٍ، إِلَّا مِنْ جَنَابَةٍ»            رواه البخاري

[Alikuwa Mtume ﷺ akituamrisha tukiwa safarini tupukuse khofu zetu, na tusizifue siku tatu, kwa kwenda haja kubwa, kukojoa na kulala isipokuwa kutokana na janab]                [Imepokewa na Bukhari.]   

Yaani mwenye janaba ni juu yake azivue khofu mbili kwa kuoga kisha azivae mara nyingine.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

8031729
TodayToday812
Highest 07-31-2026 : 9991
US
Guests 132

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a8d81be017b211567369661787658686
title_6a8d81be0180112285839311787658686
title_6a8d81be0184d611923981787658686

NISHATI ZA OFISI

title_6a8d81be164c81471524341787658686
title_6a8d81be1651518132689281787658686
title_6a8d81be165619126611981787658686 Add content here

HUDUMA MPYA

: 1 + 12 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

Go to top
UongofuUongofu.com