Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


MAANA YA KUTAYAMAMU 
Kutayamamu kilugha: Ni Kukikusudia kitu na kukielekea
Ama Maana yake kisheria: Ni Kupukusa uso na viganja vya mikono miwili kwa ardhi Twahara kwa nia ya kujitwahirisha

HUKMU YA KUTAYAMAMU
Inapasa kutayamamu yakikosekana maji au ikawa haiwezikani kuyatumia kwa jambo linalolazimu utwahara kama vile Swala. na kutayamamu kunapendekezwa katika kufanya jambo linalopendekezwa kama vile kusoma Qur'ani.

DALILI ZA KUTAYAMAMU 

Kutayamamu kumethibiti katika Qur-ani Tukufu, Sunna na Ijmaa ya Wanachuoni.

Dalili ya Kutayamamu katika Qur'ani.

1. Mwenyezi Mungu  Anasema:

 

فَلَمْ تَجِدُوا مَاءً فَتَيَمَّمُوا صَعِيدًا طَيِّبًا فَامْسَحُوا بِوُجُوهِكُمْ وَأَيْدِيكُمْ}     النساء:43}

 

[Mkitopata maji kusudieni ardhi nzuri, mpanguse nyuso zenu na mikono yenu ]    [4:43]

Ama Dalili yake katika Sunna.

2. Amesema Mtume :

 

أعطيت خمسا ، لم يعطهن أحد من الأنبياء قبلي : نصرت بالرعب مسيرة شهر ، وجعلت لي الأرض مسجدا وطهورا ، فأيما رجل من أمتي أدركته الصلاة فليصل     رواه البخاري

 

[Nimepewa mambo matano hakuna aliyepewa kabla yangu: Nimenusuriwa kwa kitisho masafa ya mwezi, nimefanyiwa ardhi kuwa ni mahali pa kuswali na pa kujitwahirishia: kwani yoyote katika umma wangu atakayeingiliwa na kipindi cha Swala na aswali]             [Imepokewa na Bukhari.].

Ama Ijmaa, wanazuoni wote wamekogomana na kukubaliana kuwa tayamamu imefanywa kuwa ni sheria, itumike badala ya ya udhu na josho katika hali na mazingira maalum yaliyobainishwa na sheria.

HEKIMA YA SHERIA KUWEKA KUTAYAMAMU

1. Kuwasahilishia umma wa Mtume Muhammad

2. Kuepusha madhara yanayosababishwa na utumiaji maji katika hali ya ugonjwa, na baridi kali na mfano wa hayo.

3. Kudumisha mafungamano ya ibada yasikatike kwa kukosekana maji, au kutoweza kuyatumia


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6785135
TodayToday136
Highest 07-17-2025 : 4917
US
Guests 24

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68a952b9b751c6713458781755927225
title_68a952b9b760514911660261755927225
title_68a952b9b76f316474188071755927225

NISHATI ZA OFISI

title_68a952b9b8c8f15090971461755927225
title_68a952b9b8d7213283904381755927225
title_68a952b9b8e5b5790996361755927225 Add content here

HUDUMA MPYA

: 13 + 14 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com