Menu

SOMO LA FIQHI


 somo lafiqhi


Suali: Ni zipi Faradhi za udhu?

Jawabu: Faradhi za Udhu ni sita
1.Kutia nia. kwa neno lake Mtume:

 

إنَّما الأَعمالُ بالنِّيَّات]    رواه البخاري]

 

[Hakika (kusihi) ibada ni kwa (kupatikana) nia]   [Imepokewa na Bukhari]

Na mahali pake ni moyoni, wala haitamkwi. Na lau mtu afanya matendo ya kutawadha kwa lengo la kujiburudisha au kujinadhifisha, bila ya nia ya kutawadha, basi hilo halimtoshelezi.

2. Kuosha uso. Na miongoni mwa huko ni kusukutua na kupaliza puani.

3. Kuosha mikono miwili pamoja na vifundo viwili.

4. Kupangusa kichwa chote, pamoja na masikio mawili

5. Kuosha miguu miwili pamoja na vifundo viwili.

Kwa neno lake Mwenyezi Mungu mtukufu:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا قُمْتُمْ إِلَى الصَّلَاةِ فَاغْسِلُوا وُجُوهَكُمْ وَأَيْدِيَكُمْ إِلَى الْمَرَافِقِ وَامْسَحُوا بِرُءُوسِكُمْ وَأَرْجُلَكُمْ إِلَى الْكَعْبَيْنِ}   المائدة:6}

 

[Enyi mlio amini! Mnapo simama kwa ajili ya Sala basi osheni nyuso zenu, na mikono yenu mpaka vifundoni, na mpake vichwa vyenu, na osheni miguu yenu mpaka vifundoni]   [Al Maaida:6]

6. Kufuatanisha beina ya viungo.

haya yamethibitika kutokana na hii Aya iliofunza juu ya udhu - Al Maida : 6, kwani “wau” iliomo kwenye Aya hii ni yenye kueleza juu ya mpangilizio. Pia haikupokewa kuwa Mtume wetu amewahi kutawadha bila ya mpangilizio kama ulivyokuja kwenye Aya hii.

Vilevile ameeleza Mtume wetu ﷺ alisema baada ya kukamilisha kutia udhu maneno yenye maana kama hivi:

 

هَذَا وُضُوءُ مَنْ لا يَقْبَلُ اللَّهُ مِنْهُ صَلاةً إِلا بِهِ]    رواه البخاري]

 

[Huu ndio udhu, hakubali Mwenyezi Mungu Mtukufu Sala ila kwa udhu kama huu]  [Imepokewa na Bukhari]


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6785141
TodayToday142
Highest 07-17-2025 : 4917
US
Guests 28

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68a952b9b751c6713458781755927225
title_68a952b9b760514911660261755927225
title_68a952b9b76f316474188071755927225

NISHATI ZA OFISI

title_68a952b9b8c8f15090971461755927225
title_68a952b9b8d7213283904381755927225
title_68a952b9b8e5b5790996361755927225 Add content here

HUDUMA MPYA

: 7 + 4 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com