Menu

SOMO LA FIQHI


 somo lafiqhi


Tukiyaangalia maji kwa kuuzingatia wingi na uchache wake tutayakuta yamegawanyika sehemu/mafungu mawili:-

1. Maji mengi, na
2. Maji machache

MAJI MENGI: Haya kwa mtazamo wa sheria ni yale yaliyofikia Qullatein na zaidi yake.

Qullatein ni miongoni mwa vipimo vilivyokuwa vikitumiwa na Waarabu zamani. Kwa vipimo tuvitumiavyo leo Qullatein ni sawa na lita 216 za ujazo.

Kwa vipimo vya ukubwa Kullatein ni sawa na dhiraa moja na robo upana, urefu na kina. Dhiraa moja ni sawa sawa na sentimeta 48 (48 cm)

 

HUKUMU YA MAJI MENGI

Maji yaliyofikia Qullatein na kuendelea hayanajisiki kwa kuingia tu najisi ndani yake bali ya kuwa yamenajisika ikiwa najisi hiyo itaharibu mojawapo ya zile sifa tatu za maji.Kwa hadithi ya bwana Mtume ﷺ:

 

   إذَا كَانَ الْمَاءُ قُلَّتَيْنِ لَمْ ، يَحْمِلْ الْخَبَثَ]    رواه أحمد إبن ماجة وغيرهما]

 

[Maji ya kifikia Qullatein haya bebi Uchafu]     [Imepokewa na Ibnu Majah na Ahmad]

Kwa Mafhumu ya hadithi hii inamanisha Maji ya kiwa ni chini ya Qullatein yanabeba Uchafu.

MAJI MACHACHE

Maji yatahukumiwa kuwa ni machache ikiwa hayakufikia kiwango cha kullatein yaani yako chini ya lita 216 za ujazo ambazo ni karibu ya madebe 12 yaliyojaa.

HUKUMU YA MAJI MACHACHE

Maji haya yatanajisika kwa kuingiwa na najisi hata kama najisi hiyo haikuharibu mojawapo ya sifa za maji, na yatahukumiwa kwa mujibu wa sheria kuwa ni maji najisi. 

KUMBUKA

Msimamo huu ni kulengana na Madh'habu ya Imamu Shafi na Imam Ahmad Mungu awerehemu,ama Imam Malik na wengineo wamesema hakuna tafauti ya Maji mengi na mai kidogo,na wakasema Maji hayanajisiki mpaka ya badilike moja katika sifa zake Rangi yake au harufu yake au ladha yake,sawa ya kiwa ni Maji mengi au maji kidogo.Na huu ndio msimamo wa Sheikhul-Islam Ibnu Taymiyah Mungu amrehemu.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6785134
TodayToday135
Highest 07-17-2025 : 4917
US
Guests 20

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68a952b9b751c6713458781755927225
title_68a952b9b760514911660261755927225
title_68a952b9b76f316474188071755927225

NISHATI ZA OFISI

title_68a952b9b8c8f15090971461755927225
title_68a952b9b8d7213283904381755927225
title_68a952b9b8e5b5790996361755927225 Add content here

HUDUMA MPYA

: 11 + 13 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com