Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


KUMTANGULIA IMAMU KATIKA SWALA

1. Amri ya Sheria ni kuwa maamuma amfuate imamu wake kwa kufanya kitendo anachofanya imamu wake papo kwa papo, kwa kauli ya Mtume ﷺ:

 

إِنَّمَا جُعِلَ الإِمَامُ لِيُؤْتَمَّ بِهِ، فَإِذَا كَبَّرَ فَكَبِّرُوا، وإِذَا سَجَدَ فَاسْجُدُوا]    رواه البخاري ومسلم]

 

[Imamu amewekwa afuatwe: akipiga takbri, na nyinyi pigeni takbiri, na akisujudu, na nyinyi sujuduni]     [ Imepokewa na Bukhari na Muslim.]

2. Imeharamishwa kumtangulia imamu, na Mtume alilitilia hilo makazo mkubwa kwa kusema:

 

أما يخشى الذي يرفع رأسه قبل الإمام أن يحول الله رأسه رأس حمار]    رواه البخاري ومسلم]

 

[Kwani haogopi ambae anaeinuwa kichwa chake kabla ya imamu, Mwenyezi Mungu amgeuze kichwa chake akifanye kichwa cha punda]    [ Imepokewa na Bukhari na Muslim.].

3. Mwenye kumtangulia imamu wake kwa kusahau itamlazimu arudi amfuate.

 

TANBIHI:

Kuswali nyuma ya asiye na Twahara
Swala Haisihi nyuma ya asiye na twahara isipokuwa iwapo hakujulishwa kuwa hana udhu mpaka baada ya kumalizika Swala. Na katika hali hii inasihi swala ya maamuma, na ni juu ya imamu arudie Swala.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6668017
TodayToday705
Highest 06-05-2025 : 6758
US
Guests 31

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_686694ca9b75916565373161751553226
title_686694ca9b83a8671383051751553226
title_686694ca9b91010505901751553226

NISHATI ZA OFISI

title_686694ca9ceca14034352851751553226
title_686694ca9cfa68478615741751553226
title_686694ca9d07e15764738281751553226 Add content here

HUDUMA MPYA

: 14 + 1 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com