Menu

SOMO LA FIQHI


 somo lafiqhi


Suali: Nipi hukumu ya swala tano?

Jawabu:  Swala tano ni wajibu kwa kila Muislamu, kulingana na Qur'ani, na Sunna na umoja wa wanavyuoni:

1. katika Qur’ani:

Anasema Mwenyezi Mungu Aliyetukuka:

 

وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَارْكَعُوا مَعَ الرَّاكِعِينَ}    البقرة:43}

 

[Na simamisheni Swala na toeni Zaka na rukuuni pamoja na wenye kurukuu]      [Al-Baqara: 43].

Na Amesema tena katika aya nyingine:

 

إِنَّ الصَّلَاةَ كَانَتْ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ كِتَابًا مَّوْقُوتًا}    النساء:103}

 

[Kwani hakika Sala kwa Waumini ni faradhi iliyo wekewa nyakati maalumu]    [Al-Nnisaai:103]

2. Na katika Sunna:

 

بني الإسلام على خمس : شهادة أن لا إله إلا الله ، وأن محمدا رسول الله ، وإقام الصلاة ، وإيتاء الزكاة ، وحج البيت ، وصوم رمضان       رواه البخاري ومسلم 

 

Amesema ﷺ:[Uislamu umejengwa juu ya nguzo tano: kushuhudia kuwa hapana mola isipokuwa Mwenyezi Mungu na kwamba Muhammad ni mja Wake na mtume wake, na kusimamisha Swala, nakutoa Zaka, nakuhiji Alkaba na kufunga mwezi wa Ramadhani] [ Imepokewa na Bukhari na Muslim.].

Na imepokewa kutoka kwa Twalhah bin ‘Ubeidillah kwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume kuhusu Uislamu, akasema :

 

خمسُ صلواتٍ في اليوم واللَّيلة]، فقال هل عليَّ غيرها؟ قال: [لا، إلاَّ أن تَطوَّع]   رواه البخاري ومسلم]

 

[Ni Swala tano mchana na usiku. Akasema: “Je, kuna nyingine zinazonilazimu sizizokuwa hizo?” Akasema: La, isipokuwa ukijitolea]    [Imepokewa na Bukhari na Muslim.].

3. Umoja wa wanavyuoni:

Umma kwa umoja wao wamekubaliana juu ya uwajibu wa Swala tano kipindi cha mchana na usiku,na kuwafikiana bila ya khitilafu yoyote kwamba swala ni mojawapo ya nguzo za Uislamu.

SWALA INAMLAZIMU NANI?

Swala inamlazimu kila Muislamu, aliyebaleghe, mwenye akili, awe mwanamume au mwanamke.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7668627
TodayToday292
Highest 04-18-2026 : 16767
US
Guests 648

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_69f18c1e68b1c15916281941777437726
title_69f18c1e68b6e20611635681777437726
title_69f18c1e68bbb7114530781777437726

NISHATI ZA OFISI

title_69f18c1e7f4018321586321777437726
title_69f18c1e7f45b21429302091777437726
title_69f18c1e7f4b612899826371777437726 Add content here

HUDUMA MPYA

: 4 + 15 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com