Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


Mambo yanayo pendekezwa kufanywa ndani ya Laylatul Qadr
1. Kufanya itikafu
Nayo ni katika kumi lote wala sio usiku wa Lailatu Al-qadr peke yake, kutoka wa A’isha radhi za Allah ziwe juu yake anasema:

 

كَانَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَعْتَكِفُ الْعَشْرَ الأَوَاخِرَ مِنْ رَمَضَانَ]      رواه البخاري ومسلم]

 

[Alikuwa Mtume ﷺ akifanya itikafu katika kumi la mwisho wa mwezi wa Ramadhani]         [Imepokewa na Bukhari na Muslim.].

2. Kusimama usiku wake hali yakuamini na kutaraji malipo
Amesema Mtume ﷺ:

 

مَنْ قَامَ رَمَضَانَ إِيمَانًا وَاحْتِسَابًا غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ]     رواه البخاري ومسلم]

 

[Atakayesimama usiku wa Lailatu Al-qadr hali ya kuwa na imani na kuridhia, husamehewa yote yaliyotangulia katika madhambi yake]    [Imepokewa na Bukhari na Muslim.].

3. Kuomba Dua:
Kutoka kwa A’isha Allah awe naye radhi Anasema:

 

يا رَسُولَ اللهِ، أرَأيْتَ إنْ عَلِمْتُ أيُّ لَيْلَةٍ لَيْلَةُ الْقَدْرِ، مَا أقُولُ فِيها؟ قَالَ: قُولي: اللَّهُمَّ إنَّكَ عَفُوٌّ كَرِيمٌ تُحِبُّ العَفْوَ فَاعْفُ عَنِّي]     رواه الترمذي]

 

[Nilisema: Ewe Mtume wa Allah, ikiniafikia Lailatu Al-qadr niombe kitu gani? Akasema: Sema: Ewe Mola! Hakika yako wewe ni mwenye kusamehe (madhambi) tena Mkarimu wapenda sana kusamehe, basi nisamehe (makosa yangu)]   [Imepokewa na Tirmidhi.].

4. Kuwaamsha watu wa nymbani kwa ajiliya ibaada
Amepokeya bibi A’isha radhi za Allah ziwe juu yake Amesema:

 

كَانَ النبي - صلى الله عليه وسلم - إِذَا دَخَلَ الْعَشْرُ شَدَّ مِئْزَرَهُ، وَأَحْيَا لَيْلَهُ، وَأَيْقَظَ أَهْلَهُ]       رواه البخاري]

 

[Alikuwa Mtume likiingia kumi la mwisho akijifunga kibwebwe na akikesha usiku wake na akiamsha wake zake]   [Imepokewa na Bukhari.]


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7669903
TodayToday1568
Highest 04-18-2026 : 16767
US
Guests 467

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_69f1ab0d75e4816461509411777445645
title_69f1ab0d75e976554340731777445645
title_69f1ab0d75ec56263797541777445645

NISHATI ZA OFISI

title_69f1ab0d7644e773638431777445645
title_69f1ab0d7649b17145090231777445645
title_69f1ab0d764e714440814531777445645 Add content here

HUDUMA MPYA

: 2 + 5 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com