Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi 


Suali: Ni nini Maana ya Saumu kilugha na kisheria

Jawabu: Maana ya Saumu Katika Lugha
Ni kujizuia na kujiepusha kufanya jambo fulani.

Ama Saumu Kisheria
Ni kufanya ibada kwa ajili ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka kwa kujizuia kula, kunywa na kufanya tendo la ndoa kuanzia kutokeza kwa alfajiri hadi kutwa kwa Jua.

 

FADHLA ZA SAUMU

 

Suali: Ni zipi Fadhla za saumu?

Jawabu: Saumu ina fadhila kubwa sana, na thawabu nyingi mno tena maradufu, na kwa hakika Mwenyezi Mungu ameinasibisha saumu kwake yeye kwa ajili ya kuipa utukufu na kuitukuza. Katika Hadithi Al-Qudsy iliyopokewa na swahaba Abu Hurayrah, Radhi za Allah ziwe juu yake  Anasema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu :

 

كُلُّ عَمَلِ ابْنِ آدَمَ يُضَاعَفُ الْحَسَنَةُ عَشْرُ أَمْثَالِهَا إِلَى سَبْعمِائَة ضِعْفٍ ، قَالَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ : إِلا الصَّوْمَ فَإِنَّهُ لِي وَأَنَا أَجْزِي بِهِ]     رواه البخاري ومسلم]

[Kila tendo la mwanadamu huongezwa malipo ya wema wake mara kumi ya mfano wa jema hilo alilolitenda mpaka hufikia kuongezwa hadi nyogeza mara sabiini. Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: Isipokuwa saumu, kwani hiyo saumu ni yangu mimi, na mimi ndiye mwenye kutoa malipo yake; (mja wangu) anaacha matamanio yake na chakula chake kwa ajili yangu. Katika kufunga saumu kuna furaha mbili: furaha (ya kwanza) ni pale anapofungua saumu aliyefunga, na furaha (ya pili) ni wakati (aliyefunga) atakapokutana na Mola wake. Na harufu inayotoka kwenye kinywa cha aliyefunga ni nzuri sana mbele ya Mwenyezi Mungu kushinda harufu ya miski]   [Imepokewa na Bukhari na Muslim.]

 

HIKMA ZA KUFARADHIWA KUFUNGA

 

Suali: Ni zipi hikma za Kufaradhiwa sumu:

Jawabu: Hekima za kufaradhishwa kufunga ni nyingi Miongani mwa hizo ni hizi
1. Ni mja kupata ucha Mungu kwa kuitika amri ya Mola wake amri hii ya kufunga na kujitolea muhanga kuitekeleza sheria ya Mola wake. Anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ}     البقرة:183}

 

[Enyi mlioamini! Mmelazimishwa kufunga (saumu) kama walivyolazimishwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Mungu]    [Al-Baqarah- Aya 183]

2. Kuipa nafsi mazoezi ya kusubiri, na kujipa nguvu ili kuweza kushinda matamanio.

3. Kujizoezesha mtu kufanya hisani, na kuwa na huruma kwa wanaohitaji masikini na mafukara; kwa sababu mtu anapoonja hisia ya njaa itampelekea mtu huyu kuwa na moyo laini na kuhisi jinsi wanavyohisi ndugu zake wahitaji wasio na chochote cha kula.

4. Kupata raha ya kiwiliwili na afya bora katika kufunga.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7887144
TodayToday277
Highest 05-20-2026 : 12580
US
Guests 32

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a3ba24a7a77d10759523161782293066
title_6a3ba24a7a7ab17664914151782293066
title_6a3ba24a7a7f721195042091782293066

NISHATI ZA OFISI

title_6a3ba24a7ad9712658378911782293066
title_6a3ba24a7ade44692338551782293066
title_6a3ba24a7ae2f1520320601782293066 Add content here

HUDUMA MPYA

: 5 + 13 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com