Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


Hukumu ya kuzuru Msikiti wa Mtume ﷺ

Kuuzuru Msikiti wa Mtume si miongoni mwa masharti ya Hija wala nguzo zake wala wajibu zake. Hilo ni sunna, na inafaa ifanywe wakati wowote.

Na ni wajibu liwe lengo la ziara ni kuswali kwenye huo Msikiti na sio kaburi. Abu Huraira Radhi za Allah ziwe juu yake amepokewa akisema kumpokea Mtume kuwa alisema:

 

لَا تُشَدُّ الرِّحَالُ إِلَّا إِلَى ثَلَاثَةِ مَسَاجِد: الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ، وَمَسْجِدِ الرَّسُولِ ﷺ ، وَالمَسْجِدِ الأَقْصَى]    رواه مسلم]

 

[Hakufungwi safari isipokuwa kwenda kwenye misikiti mitatu: Msikiti wa Haram, Msikiti wa Mtume na Msikiti wa Aqswa]    [Imepokewa na Muslim.].

Amesema Shekhe wa Uislamu Ibnu Taimiyya: “Iwapo lengo lake la safari ni kuzuru kaburi ya Mtume na sio kuswali kwenye Msikiti wake…. Basi msimamo wa maimamu na wengi wa wanavyuoni ni kuwa hili halikuwekwa na Sheria wala halikuamrishwa…Na Hadithi kuhusu kuzuru kaburi ya Mtume zote ni dhaifu kwa itifaki ya wajuzi wa Hadithi, bali ni Hadithi zilizobuniwa. Hakuna yoyote miongoni mwa wakusanyaji wa Vitabu vya Sunna za Mtume aliyepokea Hadithi hizo, na hakuna yoyote aliyesimamisha hoja kutegemea hadithi yoyote katika hizo” [Majmuu’ al- Fataawaa, juzu. ii, uk. 26].


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7887141
TodayToday274
Highest 05-20-2026 : 12580
US
Guests 40

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a3ba1d50805a8082642291782292949
title_6a3ba1d5080a93861093361782292949
title_6a3ba1d5080f521120081921782292949

NISHATI ZA OFISI

title_6a3ba1d5086c84043400041782292949
title_6a3ba1d50871513912395201782292949
title_6a3ba1d50876f6710584861782292949 Add content here

HUDUMA MPYA

: 15 + 5 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com