Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


Hukumu ya kuzuru Msikiti wa Mtume ﷺ

Kuuzuru Msikiti wa Mtume si miongoni mwa masharti ya Hija wala nguzo zake wala wajibu zake. Hilo ni sunna, na inafaa ifanywe wakati wowote.

Na ni wajibu liwe lengo la ziara ni kuswali kwenye huo Msikiti na sio kaburi. Abu Huraira Radhi za Allah ziwe juu yake amepokewa akisema kumpokea Mtume kuwa alisema:

 

لَا تُشَدُّ الرِّحَالُ إِلَّا إِلَى ثَلَاثَةِ مَسَاجِد: الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ، وَمَسْجِدِ الرَّسُولِ ﷺ ، وَالمَسْجِدِ الأَقْصَى]    رواه مسلم]

 

[Hakufungwi safari isipokuwa kwenda kwenye misikiti mitatu: Msikiti wa Haram, Msikiti wa Mtume na Msikiti wa Aqswa]    [Imepokewa na Muslim.].

Amesema Shekhe wa Uislamu Ibnu Taimiyya: “Iwapo lengo lake la safari ni kuzuru kaburi ya Mtume na sio kuswali kwenye Msikiti wake…. Basi msimamo wa maimamu na wengi wa wanavyuoni ni kuwa hili halikuwekwa na Sheria wala halikuamrishwa…Na Hadithi kuhusu kuzuru kaburi ya Mtume zote ni dhaifu kwa itifaki ya wajuzi wa Hadithi, bali ni Hadithi zilizobuniwa. Hakuna yoyote miongoni mwa wakusanyaji wa Vitabu vya Sunna za Mtume aliyepokea Hadithi hizo, na hakuna yoyote aliyesimamisha hoja kutegemea hadithi yoyote katika hizo” [Majmuu’ al- Fataawaa, juzu. ii, uk. 26].


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6785517
TodayToday518
Highest 07-17-2025 : 4917
US
Guests 29

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68a98fb749eac19585245311755942839
title_68a98fb749fa912203850161755942839
title_68a98fb74a09319110417461755942839

NISHATI ZA OFISI

title_68a98fb74d9605821471001755942839
title_68a98fb74da5c17044642991755942839
title_68a98fb74db3b13656295111755942839 Add content here

HUDUMA MPYA

: 9 + 15 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com