Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


Majina ya mji wa Mtume wa Madina
1. Madina:
Amesema Mwenyezi Mungu Aliyetukuka

 

8:يَقُولُونَ لَئِن رَّجَعۡنَآ إِلَى ٱلۡمَدِينَةِ لَيُخۡرِجَنَّ ٱلۡأَعَزُّ مِنۡهَا ٱلۡأَذَلَّۚ}   المنافقون}

 

[Wanasema: lau tutarudi Madina watawatoa walio watukufu zaidi wale walio wanyonge zaidi]    [63: 8].

2. Twaba:
Amepokewa Jabir bin Samurah Radhi za Allah ziwe juu yake akisema:

 

إِنَّ الله تَعَالَى سَمَّى الْمَدِينَةَ طَابَةَ]     رواه مسلم]

 

[Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu  akisema: [Hakika Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Ameipa Madina jina la Twaba]   [Imepokewa na Muslim.].

3. Twayiba:
Amepokewa Zaid bin Tahabit Radhi za Allah ziwe juu yake akisema akipokea kutoka Mtume (saw) akisema:

 

إِنَّهَا طَيْبَةُ، تَنْفِي الذُّنُوبَ كَمَا تَنْفِي النَّارُ خَبَثَ الْفِضَّةِ]    متفق عليه]

 

[Hiyo ni Twayiba, inaondoa dhambi kama ambapo moto unaondoa uchafu wa fedha] [Imepokewaq na Bukhari na Muslim.].

Fadhila za mji wa Mtume

1. Sa'ad bin Abii Waqqaasw Radhi za Allah ziwe juu yake amepokewa akisema kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema:

 

الْمَدِينَةُ خَيْرٌ لَهُمْ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ، لَا يَدَعُهَا أَحَدٌ رَغْبَةً عَنْهَا إِلَّا أَبْدَلَ الله فِيهَا مَنْ هُوَ خَيْرٌ مِنْهُ، وَلَا يَثْبُتُ أَحَدٌ عَلَى لَأْوَائِهَاِ  وَجَهْدِهَا إِلَّا كُنْتُ لَهُ شَفِيعًا أَوْ شَهِيدًا يَوْمَ الْقِيَامَةِ 

[Madina ni bora kwao lau walikuwa wanajua. Haiachi mtu yoyote kwa kutoipenda isipokuwa Mwenyezi Mungu humweka mtu bora kuliko yeye awe ni badala yake. Na yoyote atakayevumilia shida zake na usumbufu wake, nitakuwa ni muombezi wake au shahidi wake Siku ya Kiyama]    [Imepokewa na Muslim.].

2. Abu Huraira Radhi za Allah ziwe juu yake amepokewa akisema kwamba Mtume amesema:

 

أُمِرْتُ بِقَرْيَةٍ تَأْكُلُ الْقُرَى يَقُولُونَ يَثْرِبُ وَهْيَ الْمَدِينَةُ، تَنْفِي النَّاسَِ كَمَا يَنْفِي الْكِيرِ خَبَثَ الْحَدِيدِِ.]  متفق عليه]

 

[Nimeamrishwa kwenye kitongoji (nimeamrishwa nigurie hapo, niteremkie hapo na niishi hapo.) kinachokula vitongoji (watu wake wata washinda watu wa miji mingine na kitakuwa ni kituo cha majeshi ya Kiislamu.), wanakiita Yathrib, nayo ni Madina, inawaondoa watu , kama vile kiriba kinvyoondoa uchafu wa chuma]  [Imepokewa na Bukhaeri na Muslim.].


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7887015
TodayToday148
Highest 05-20-2026 : 12580
US
Guests 67

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a3b8054cd98317216541681782284372
title_6a3b8054cd9d217445950591782284372
title_6a3b8054cda1f1767755151782284372

NISHATI ZA OFISI

title_6a3b8054cdfae15514579881782284372
title_6a3b8054cdffb16119036301782284372
title_6a3b8054ce04610836102901782284372 Add content here

HUDUMA MPYA

: 3 + 13 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com