Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi 


Suali: Ni nini Maana ya Umra

Jawabu: Maana ya Umra Umra kilugha ni Ziara

Ama maana yake kisheria 
Ni kuizuru Nyumba Takatifu (Alkaba) wakati wowote mtu anapotaka, kwa kutekeleza matendo ya ibada maalumu.

Suali: Ni ipi Hukumu ya Umra na fadhla zake
Jawabu: Umra ni wajibu wa mara moja katika umri kama vile hajji. Kwa neno lake Mwenyezi Mungu aliyetukuka:

 

وَأَتِمُّوا الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ لِلَّهِ}    البقرة:196}

 

[Na timizeni Hija na 'Umra kwa ajili ya Mwenyezi Mungu].     [Al Baqara : 196]

Na kwa kauli yake Mtume ﷺ :

 

الإسلام أن تشهد أن لا إله إلا الله وأن محمدا رسول الله ، وتقيم الصلاة ، وتؤتي الزكاة ، وتحج البيت وتعتمر ، وتغتسل من الجنابة ، وتتم الوضوء ، وتصوم رمضان )   رواه إبن خزيمة والدار قطني, وقال الدارقطني : هذا إسناد ثابت صحيح

[Uislamu ni ukubali kwamba hakuna mola isipokuwa Mwenyezi Mungu na kwamba Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu, na usimamishe Swala, na utoe Zaka, na uikusudie Alkaba kwa ibada ya Hija na ufanye Umra, na uoge kutokana na janaba, na ukamilishe udhu, na ufunge Ramadhani] [Imepokewa na Ibnu Khuzaimah na AL-Ddaar Qutiniy na akasema isnadi yake ni thaabit na nisahihi]

Na amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ:

 

  العمرة إلى العمرة كفارة لما بينهما والحج المبرور ليس له جزاء إلا الجنة]     رواه البخاري ومسلم]

 

[Umra mpaka Umra ni kafara ya dhambi baina yake, na Hija iliyokubaliwa haina malipo isipokuwa Pepo]       [Imepokewa na Bukhari na Muslim.]


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6668042
TodayToday730
Highest 06-05-2025 : 6758
US
Guests 23

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68669c122122619976556121751555090
title_68669c12213108441554001751555090
title_68669c12213f611807435721751555090

NISHATI ZA OFISI

title_68669c12229e915233395891751555090
title_68669c1222ac51836088421751555090
title_68669c1222b9b10634934991751555090 Add content here

HUDUMA MPYA

: 6 + 10 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com