Menu

 

HUKMU YA MWANAMUME KUVAA CHENI

Suali: ni ipi hukmu ya Mwanamume kuvaa cheni ya Fedha? 

Jawabu: Mwanamume kuvaa cheni au vipuli kwa ajili ya mapambo haifai na ni haramu kuvaa mapambo kama hayo, sawa iwe ni za fedha au madini mengine yoyote kwa sababu ni kujifananisha na wanawake na Mtume amemlaani mwanamume mwenye kujifananisha na wanawake na mwanamke mwenye kujifananisha na mwanamume kama ilivyo kuja kwenye hadithi iliyopokelewa na Imamu Al Bukahri:

 

[لَعَنَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ الْمُتَشَبِّهِينَ مِنْ الرِّجَالِ بِالنِّسَاءِ وَالْمُتَشَبِّهَاتِ مِنْ النِّسَاءِ بِالرِّجَالِ]

 

[Amemlaani Mtume wa Mwenyezi Mungu wanaume wanao jifananisha na wanawake,na wanawake wanao jifananisha na wanaume]

Na imekuja Hadithi iliyopokelewa na Abuu Hurayra radhi za Allah ziwe juu yake asema:

 

لَعَنَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ الرَّجُلَ يَلْبَسُ لِبْسَةَ الْمَرْأَةِ وَالْمَرْأَةَ تَلْبَسُ لِبْسَةَ الرَّجُلِ]    رواه أبوداود]

 

[Amemlaani Mtume wa Mwenyezi Mungu Mwaname anaevaa vazi la wanawake na Wanawake wanao vaa mavazi ya wanamume].    [Imepokewa na Abuu Daud].

Na wanazuoni wameweka qaaida maluum kuhusu mavazi na mapambo wakasema chochote kinacho julikana kuwa ni katika matumizi ya wanawake peke yao basi ni haramu kwa mwanamume kutumia kama kuvaa mkufu bangili, vipuli na kadhalika.

Na mwanamume anaruhusiwa kuvaa pete ya fedha kama ilivyo pokelewa katika sahih Al Bukharin a Muslim kuwa mtume alikuwa na pete ya Fedha.
Na Allah ndie mjuzi zaidi


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6707902
TodayToday834
Highest 07-09-2025 : 5269
US
Guests 26

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_687bd498d056711726399611752945816
title_687bd498d065218162061251752945816
title_687bd498d07346420555341752945816

NISHATI ZA OFISI

title_687bd498d1cc04511089601752945816
title_687bd498d1da310126118251752945816
title_687bd498d1e8413797462731752945816 Add content here

HUDUMA MPYA

: 9 + 15 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com