Menu

 

HUKMU YA MWANAMUME KUVAA CHENI

Suali: ni ipi hukmu ya Mwanamume kuvaa cheni ya Fedha? 

Jawabu: Mwanamume kuvaa cheni au vipuli kwa ajili ya mapambo haifai na ni haramu kuvaa mapambo kama hayo, sawa iwe ni za fedha au madini mengine yoyote kwa sababu ni kujifananisha na wanawake na Mtume amemlaani mwanamume mwenye kujifananisha na wanawake na mwanamke mwenye kujifananisha na mwanamume kama ilivyo kuja kwenye hadithi iliyopokelewa na Imamu Al Bukahri:

 

[لَعَنَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ الْمُتَشَبِّهِينَ مِنْ الرِّجَالِ بِالنِّسَاءِ وَالْمُتَشَبِّهَاتِ مِنْ النِّسَاءِ بِالرِّجَالِ]

 

[Amemlaani Mtume wa Mwenyezi Mungu wanaume wanao jifananisha na wanawake,na wanawake wanao jifananisha na wanaume]

Na imekuja Hadithi iliyopokelewa na Abuu Hurayra radhi za Allah ziwe juu yake asema:

 

لَعَنَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ الرَّجُلَ يَلْبَسُ لِبْسَةَ الْمَرْأَةِ وَالْمَرْأَةَ تَلْبَسُ لِبْسَةَ الرَّجُلِ]    رواه أبوداود]

 

[Amemlaani Mtume wa Mwenyezi Mungu Mwaname anaevaa vazi la wanawake na Wanawake wanao vaa mavazi ya wanamume].    [Imepokewa na Abuu Daud].

Na wanazuoni wameweka qaaida maluum kuhusu mavazi na mapambo wakasema chochote kinacho julikana kuwa ni katika matumizi ya wanawake peke yao basi ni haramu kwa mwanamume kutumia kama kuvaa mkufu bangili, vipuli na kadhalika.

Na mwanamume anaruhusiwa kuvaa pete ya fedha kama ilivyo pokelewa katika sahih Al Bukharin a Muslim kuwa mtume alikuwa na pete ya Fedha.
Na Allah ndie mjuzi zaidi


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

8031725
TodayToday808
Highest 07-31-2026 : 9991
US
Guests 123

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a8d80d7693f58905492441787658455
title_6a8d80d76944413991232981787658455
title_6a8d80d76949215784487081787658455

NISHATI ZA OFISI

title_6a8d80d769a3010101924721787658455
title_6a8d80d769a7d14357852021787658455
title_6a8d80d769ac86460858161787658455 Add content here

HUDUMA MPYA

: 14 + 14 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

Go to top
UongofuUongofu.com