Menu

HUKMU YA KUVUTA SHISHA

 

SUALI: Ni ipi hukmu ya kuvuta shisha?

 

JAWABU: Kuvuta shisha ni haramu kama vile kuvuta sigara, kwa kupatikana madhara mengi,kwanza kujidhuru katika nafsi yake,na kwa kupoteza mali yake,na kwa kuwadhuru wenzake. Sharia yetu imekuja kuharamisha kila baya na lenye na madhara.

Mwenyezi Mungu anasema kuhusu hikma ya kumtumiliza Mtume:

 

وَيُحِلُّ لَهُمُ الطَّيِّبَاتِ وَيُحَرِّمُ عَلَيْهِمُ الْخَبَائِثَ}    الأعراف:157}

 

"Na anawahalalishia vizuri, na ana waharimishia viovu."     [Al-A'araaf:157]

Na imethubutu kiilimu kuwa uvutaji wa shisha na sigara,kunasababisha maradhi mabaya yenye kuamgamiza, na Mwenyezi mungu amesema:

وَلَا تَقْتُلُوا أَنفُسَكُمْ ۚ إِنَّ اللَّهَ كَانَ بِكُمْ رَحِيمًا}       النساء:29}

 

"Wala msijiuwe. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwarehemuni.       [Al-Nnisaa:29

Na yoyote mwenye kutumia uraibu huo huhesabiwa amejidhulumu nafsi yake,na kuwadhuru wanao kaa karibu na yeye. Kwa hivyo uvutaji wa sigara na shisha ni katika madhambi makubwa ni lazima kwa anae tumia uraibu huu uraibu afanye bidii kuwacha na kutubia kwa Mwenzi Mungu, na kumuomba Allah amsaidie kuweza kuwacha.
Na bila shaka uvutaji wa sigara ni katika mitihani mikubwa ilio wakumba waislamu. Kiasi ya kuwa asilimia kubwa katika waislamu hutumia sigara na kuonekana ni jambo la kawaida.

Na allah ndie mjuzi zaidi.

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7669204
TodayToday869
Highest 04-18-2026 : 16767
US
Guests 211

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_69f19b72651c410087629061777441650
title_69f19b726521411237303111777441650
title_69f19b72652613903890491777441650

NISHATI ZA OFISI

title_69f19b7265801128810641777441650
title_69f19b726584f13757718421777441650
title_69f19b726589c15174479651777441650 Add content here

HUDUMA MPYA

: 1 + 15 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com