Menu

NI MAMBO GANI ANATAKIWA KUFANYA MWANAMKE ALIE KWENYE EDA YAKUFILIWA?


Suala:

Mwanamke aliefiliwa na Mumewe ni mambo gani yanaomlazimu kufanya?


Jawabu:
Ni wajibu kwa mwanamke aliefiwa na mumewe kuomboleza katika muda wa eda , na kuomboleza ina hukmu ambazo ni lazima kuzichunga, tutazifupisha katika mambo matano:
Kwanza : kujilazimisha kukaa katika nyumba yake ambayo anaishi ndani yake wakati wa kifo cha mumewe , hivyo basi atakaa katika nyumba hiyo mpaka kukamilika kwa eda yake ,nayo ni miezi minne na siku kumi kwa neno lake Mwenyezi Mungu aliposema:

 

[ والذين يتوفون منكم ويذرون أزواجاً يتربصن بأنفسهن أربعة أشهر وعشراً } [البقرة: 234}

 

[Na wale miongoni mwenu wanao kufa na wakaacha wake, hawa wake wangoje peke yao miezi mine na siku kumi.]   [Baqara:234]

Isipokua akiwa mja mzito basi eda yake itaisha pale atakapojifungua kwa neno lake Mwenyezi Mungu aliposema:

 

[4:وأولات الأحمال أجلهن أن يضعن حملهن }    [الطلاق}

 

[Na wenye mimba eda yao mpaka watakapo zaa]  [Twalaq:4]

na hatotoka katika nyumba yake isipokua kwa haja au dharura kama vile kwenda hospitalini kupata matibabu, na kununua vitu anavyovihitaji sokoni kama vile chakula na venginevyo , ikiwa hana wa kumfanyia hivyo.
Pili : Haifai kwake kuvaa nguo nzuri (asivae nguo ambazo zinahesabika ni nguo za mapambo)
Tatu :Asijipambe kwa mapambo ya aina yote kutokana na dhahabu na fedha , na almasi na lulu na mapambo mengine, sawa yawe ni mikufu au bangili au mengineo mpaka eda iishe.
Nne :Asitumie manukato ya aina yeyote sawa yawe Manukato ya kujifukiza au ya Mafuta isipokua atakapojitwahirisha kutokana na hedhi basi itambidi yeye atumie manukato katika sehemu yenye harufu mbaya.
Tano:Asijipambe katika uso wake na macho yake kwa aina yeyote ya mapambo au wanja ,na yale mambo ambayo mwenzako anaweza kukufanyia bila ya wewe kutoka basi mwachie yeye akufanyie ikiwa ukifanya wewe utalazimika kutoka.
Wala hakuna tatizo wewe kuongea na wanaume madamu mazungumzo hayo yapo ndani ya mipaka ya Adabu na heshima , Isipokua makatazo yamekuja katika kulegeza sauti Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema:

 

[فلا تخضعن بالقول فيطمع الذي في قلبه مرض}    [الأحزاب:32}

 

[basi msiregeze sauti zenu, akaingia tamaa mwenye maradhi katika moyo wake] [Ahzaab:32]

na inapaswa ifahimike yakwamba mazungumzo ya mwanamke na mwanamume inatakiwa iwe katika mipaka ya haja , na jambo hilo halina uhusiano wowote na eda, na ukitokea ukiukaji wowote kutoka kwa mwenye kukaa eda na akafanya ambalo ilimpasa aliepuke basi itambidi aombe msamaha kwa Mwenyezi Mungu na atubie na asirudie tena mambo hayo , na hana kafara isipokua hilo.
Na ALLAH ni mjuzi zaidi


*Chanzo:ISLAMWEB.NET

Imefasiriwa na Mahamd Fadhil El Shiraziy

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7887141
TodayToday274
Highest 05-20-2026 : 12580
US
Guests 39

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a3ba1cfa9b601374247341782292943
title_6a3ba1cfa9bb15254438121782292943
title_6a3ba1cfa9bfd2365691661782292943

NISHATI ZA OFISI

title_6a3ba1cfaa1be15298726751782292943
title_6a3ba1cfaa20b2952490631782292943
title_6a3ba1cfaa2578263644751782292943 Add content here

HUDUMA MPYA

: 4 + 14 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com