Menu

KWA BANU SA'AD


 b60


Siku hizo ilikuwa ni mazoea ya watu wa mijini katika Waarabu kuwatafutia watoto wao wanyonyeshaji wa mashambani ili kuwaepusha watoto wao na magonjwa ya mijini, ill iwe na nguvu miili yao, ikazane mishipa yao na waweze kukisema Kiarabu fasaha katika utoto wao.Abdul Muttwalib akamtafutia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu  wanyonyeshaji. Alimtaka mwanamke mmoja kutoka katika ukoo wa Saad bin Bakri, Halima binti Abi Dhuayb amnyonyeshe Mtume.Mume wa bibi huyu alikuwa ni Al- Harithi bin Abdil-Uzaa aliyekuwa akijulikana kwa jina la Abi Kabshah kutoka katika kabila hilo hilo.
Ndugu zake Mtume wa kunyonya kutoka kwa mama huyo ni, Abdallah bin Al-Harithi, Unaysah binti Al- Harithi Hadhafa au Sudhamah binti Al-Harithi (na huyu ndiye Al-Shaymaa na hili ndilo jina lililoeleweka zaidi mijini kuliko hata jina lake halisi) naye alikuwa ni mmoja kati ya waliokuwa wakimlea Mjumbe wa Mwenyezi Mungu na Abu Sufyan bin Al-Harithi Bin Abdul Muttwalib, mtoto wa Ammi ya Mtume
Ammi ya Mtume Hamza Bin Abdul Muttwalib alikuwa amenyonyeshwa kwa Banu Saad bin Bakri, mama yake alimnyonyesha Mjumbe wa Mwenyezi Mungu siku moja wakati akiwa kwa mama yake Halima. Kwa hivyo,Hamza alikuwa ni mshirika na Mjumbe wa Mwenyezi Mungu katika kunyonya kwa sehemu mbili, sehemu ya Thuwayba na sehemu ya Al-Saadiyya.


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7668189
TodayToday7952
Highest 04-18-2026 : 16767
US
Guests 266

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_69f17e596893e7032680111777434201
title_69f17e596899c17808596431777434201
title_69f17e59689f415620374401777434201

NISHATI ZA OFISI

title_69f17e597f1c44636678961777434201
title_69f17e597f22e16338757781777434201
title_69f17e597f28d10863717641777434201 Add content here

HUDUMA MPYA

: 8 + 5 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com