Menu

KWA BANU SA'AD


 b60


Siku hizo ilikuwa ni mazoea ya watu wa mijini katika Waarabu kuwatafutia watoto wao wanyonyeshaji wa mashambani ili kuwaepusha watoto wao na magonjwa ya mijini, ill iwe na nguvu miili yao, ikazane mishipa yao na waweze kukisema Kiarabu fasaha katika utoto wao.Abdul Muttwalib akamtafutia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu  wanyonyeshaji. Alimtaka mwanamke mmoja kutoka katika ukoo wa Saad bin Bakri, Halima binti Abi Dhuayb amnyonyeshe Mtume.Mume wa bibi huyu alikuwa ni Al- Harithi bin Abdil-Uzaa aliyekuwa akijulikana kwa jina la Abi Kabshah kutoka katika kabila hilo hilo.
Ndugu zake Mtume wa kunyonya kutoka kwa mama huyo ni, Abdallah bin Al-Harithi, Unaysah binti Al- Harithi Hadhafa au Sudhamah binti Al-Harithi (na huyu ndiye Al-Shaymaa na hili ndilo jina lililoeleweka zaidi mijini kuliko hata jina lake halisi) naye alikuwa ni mmoja kati ya waliokuwa wakimlea Mjumbe wa Mwenyezi Mungu na Abu Sufyan bin Al-Harithi Bin Abdul Muttwalib, mtoto wa Ammi ya Mtume
Ammi ya Mtume Hamza Bin Abdul Muttwalib alikuwa amenyonyeshwa kwa Banu Saad bin Bakri, mama yake alimnyonyesha Mjumbe wa Mwenyezi Mungu siku moja wakati akiwa kwa mama yake Halima. Kwa hivyo,Hamza alikuwa ni mshirika na Mjumbe wa Mwenyezi Mungu katika kunyonya kwa sehemu mbili, sehemu ya Thuwayba na sehemu ya Al-Saadiyya.


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6785133
TodayToday134
Highest 07-17-2025 : 4917
US
Guests 18

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68a952b9b751c6713458781755927225
title_68a952b9b760514911660261755927225
title_68a952b9b76f316474188071755927225

NISHATI ZA OFISI

title_68a952b9b8c8f15090971461755927225
title_68a952b9b8d7213283904381755927225
title_68a952b9b8e5b5790996361755927225 Add content here

HUDUMA MPYA

: 3 + 11 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com