Menu

HUKMU YA KUVAA NIQAAB KATIKA IBADA YA UMRA NA HAJJI


SWALI: Nini hukumu ya mwanamke alie hirimia umra kisha akavaa Niqaab na kufinika uso wake?

JAWABU: Mwanamke akihirimia ibada ya umra au hajji huwa haifai kufinika uso wake kwa kuvaa niqaab au kuvaa soksi za mikono,kama ilivyo kuja katika hadithi ya Mtume kuhusu Mwanamke alie hirimia

 

 

عن ابن عمر رضي الله عنهما أن رسول صلى الله عليه وسلم قال : " لاتنتقب المرأة المحرمة ولا تلبس القفازين " . رواه البخاري

 

Kutoka kwa Ibnu Umar radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake kwamba Mtume amesema: [Asivae niqaabu  mwanamke alie kwenye ihramu na asivae soksi za mikono]    [imepokewa na Bukhari]
Lakini ikiwa atafunika uso wake kwa kutojua hukmu yake au kwa kusahau atakuwa hawajibiki na kitu chochote ,lakini kama alikuwa anajua basi atakuwa na khiyari kufanya moja katika mambo matatu,ima afunge siku tatu,au alishe masikini sita kila maskini nusu ya pishi,au achinje mbuzi na aigawe nyama yake kwa masikini wa mji wa makkah.

Na Mwenyezi Mungu ndie mjuzi zaidi.


 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7669220
TodayToday885
Highest 04-18-2026 : 16767
US
Guests 213

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_69f19bd81f44413997826411777441752
title_69f19bd81f4a89435856601777441752
title_69f19bd81f5061662848321777441752

NISHATI ZA OFISI

title_69f19bd81fd3f9751877821777441752
title_69f19bd81fd9f18836234721777441752
title_69f19bd81fdfc7957578371777441752 Add content here

HUDUMA MPYA

: 14 + 11 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com