Menu

MALEZI NA DOTKOMU


 babyoncomp


Sote tunafahamu matatizo yanayo kumba ulimwengu kwasababu ya utandawazi na mrupuko wa maarifa kwa sababu ya mawasiliano yalivyo kuwa rahisi kupitia runinga rununu na mitandao ya wazi. Ni vigumu sana kuhifadhi tabia za watoto katika mazingira haya. 

Tutafanya vipi kama wazazi kuwahami watoto wetu na maafa kama haya.
1. Kuelewa tunaisha katika ulimwengu aina gani na zile biri zinazotukabili katika malezi kila uchao. Kwa kufahamu aina za hatari zilizoko mbele yetu zinazoengezeka kila siku kuwa ulimwengu umekuwa kama kijiji kimoja mila na desturi za watu wengine zinapiga vita maadili ya mazuri ya jamii zetu za kiislamu.
2. Kuweka kinga za kujiepusha na uchafu na fikra mbovu zinazopatikana katika mitandao na kutahadharisha watoto wetu juu ya ubaya unaoletwa na utamaduni huu ya mawasiliano ya teknilojia kuwa rahisi na khatari zake.
3. Kuwa mbadala kwa njia ya kuwashajiisha na kuwafanaya kupenda mazuri yanayopatikana ndani ya hiyo teknolojia na kuwafanya watumie maarifa yale kwa kuboresha tabia njema,kuelimika na kueleimisha wengine. Mfano wa www.eDialogue.org mtandao ambao umewezesha kusilimisha Zaidi ya watu elfu kumi na pia nyaraka wa uso wa kitabu facebook na kiwingu skype na pia nena whatsapp.zote hizi zinaweza kutumika kwa maslahi ya Da'wa.  
a.kueneza Uislamu
b.kuelimisha watu
c.kukataza mabaya
d.kueneza tabia njema
e.kuunga kizazi
f.kuleta umoja wa waislamu
g.kupinga ufisadi
4. kuwepo na ufuatiliziaji na kutathmini miondoko yao ili wasiweze kuchukuliwa na wimbi la ufisadi na fikra potofu na kuingia katika makundi ya kigaidi.
5. Mzazi kuishi ulimwengu wa kileo wa teknolojia ajue yanayoendelea katika mitandao ya wazi kwa mfano facebook uso wa kitabu. Ili aweze kuona mtoto wake anafikiria vipi kuelekea wapi au kushirikiana na kina nani na anasoma nini katika mtandao.
6. Wazazi washirikiane kuanda makongamano ya watoto, safari za pamoja yenye kukusanya mapumziko pamoja na kujitolea kutumikia jamii. Khaswa katika likizo za shule.
7. Mzazi kujua rafiki wa watoto wake kujua wanaenda wapi wanafanya nini na kusoma nini na mipango gani ili aweze kumtahadharisha mtoto na marafiki wabaya.
8. Kuwa karibu na mtoto kwa kuwa rafiki wa mtoto wako na kusuhubiana nayeye kwa kumonesha mapenzi pasina kumnyima uhuru wake kama mtoto.

Imeandikwa na 

Sheikh Abuu Hamza

Mombasa- Kenya.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7668624
TodayToday289
Highest 04-18-2026 : 16767
US
Guests 587

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_69f18bfce18fe18548029301777437692
title_69f18bfce195011096893801777437692
title_69f18bfce19a57064357571777437692

NISHATI ZA OFISI

title_69f18bfce201f8701409581777437692
title_69f18bfce206d1320993571777437692
title_69f18bfce20b917051795171777437692 Add content here

HUDUMA MPYA

: 12 + 6 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com