Menu

BUSTANI YA WATU WEMA


1463655589


وعن حُذيْفَة بنِ الْيمانِ ، رضي اللَّه عنه ، قال: حدثنا رسولُ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم ، حَديثْين قَدْ رَأَيْتُ أَحدهُمَا ، وَأَنَا أَنْتظرُ الآخَرَ : حدَّثَنا أَنَّ الأَمَانَة نَزلتْ في جَذْرِ قُلُوبِ الرِّجَالِ ، ثُمَّ نَزَلَ الْقُرآنُ فَعلموا مِنَ الْقُرْآن ، وَعلِمُوا مِنَ السُّنَّةِ ، ثُمَّ حَدَّثنا عَنْ رَفْعِ الأَمانَةِ فَقال : «يَنَـامُ الرَّجل النَّوْمةَ فَتُقبضُ الأَمَانَةُ مِنْ قَلْبِهِ ، فَيظلُّ أَثَرُهَا مِثْلَ الْوَكْتِ ، ثُمَّ ينامُ النَّوْمَةَ فَتُقبضُ الأَمَانَةُ مِنْ قَلْبِهِ ، فَيظَلُّ أَثَرُهَا مِثْل أثرِ الْمَجْلِ ، كجَمْرٍ دَحْرجْتَهُ عَلَى رِجْلكَ ، فَنفطَ فتَراه مُنْتبراً وَلَيْسَ فِيهِ شَيءٌ » ثُمَّ أَخذَ حَصَاةً فَدَحْرجَهَا عَلَى رِجْلِهِ ، فَيُصْبحُ النَّاسُ يَتبايَعونَ ، فَلا يَكادُ أَحَدٌ يُؤدِّي الأَمَانَةَ حَتَّى يُقَالَ : إِنَّ في بَنِي فَلانٍ رَجُلاً أَمِيناً ، حَتَّى يُقَالَ لِلَّرجلِ : مَا أَجْلدهُ مَا أَظْرَفهُ ، مَا أَعْقلَهُ ، وَمَا في قلْبِهِ مِثْقَالُ حَبَّةٍ مِنْ خَرْدَلِ مِنْ إِيمانٍ. وَلَقَدْ أَتَى عَلَيَّ زَمَانٌ وَمَا أُبَالِي أَيُّكُمْ بايعْتُ ، لَئِنْ كَانَ مُسْلماً ليردُنَّهُ عَليَّ دِينُه ، ولَئِنْ كَانَ نَصْرانياً أَوْ يَهُوديًّا لَيُرُدنَّهُ عَلَيَّ سَاعِيه ، وأَمَّا الْيَوْمَ فَما كُنْتُ أُبايُعُ مِنْكمْ إِلاَّ فُلاناً وَفلاناً »     متفقٌ عليه


Kutoka kwake Hudhayfa bin Al-Yamaani Radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Ametuhadithia Mtume Hadithi mbili, nami nimeiona Hadithi moja kati ya hizo mbili na ninangoja kuiona hiyo ya pili. Alituhadithia ya kwamba, amana iliteremshwa na kukita katika mioyo ya watu. kisha iliteremshwa Qur'ani waliweza kuelimishwa kwa Qur'ani na kuelemishwa na Sunna. Kisha akatuhadithia kuhusu kunyanyuliwa Amana, akasema: [Analala mtu usiku na anapoamka na anajikuta kuwa amatolewa uaminifu katika moyo wake na kubakishwa kivuli chake tu. Kisha analala tena usiku na uaminifu unaondolewa katika moyo wake na kubakia alama ndogo mfano wa lenge lenge kama kaa la moto anapolizungusha kwa mguu wako, na hivyo kupata lenge lenge ambalo linapasuka basi ndani huwa tupu kabisa.] Kisha akachukua vijiwe na kuzigeuza kwenye mguu wake, Watu watakuwa wanauziana (katika biashara), lakini hakuna hata mmoja atayetekeleza Amana, mpaka imesemwe, hakika katika ukoo wa watu fulani kuna mtu muaminifu,(kwa kukosekana watu waminifu) pia mpaka isemwe kwa mtu (ambaye ni hodari katika mambo ya dunia). Tazama jinsi gani alivyo hodari kwenye kazi yake, jinsi gani alivyo mzuri, na jinsi gani alivyo na akili, lakini kwenye moyo wake hana hata chembe ya Imani.” Hakika nimefikiwa na wakati ambapo sikujali mtu gani ninayefanya naye biashara. Akiwa ni Musilamu basi Dini yake ni dhamana tosha kwangu,(ya kuipata haki yangu) na akiwa ni Mnaswara, au Myahudi  basi walii wake atatimiza amana hiyo (kwa kuwa ndie mdhamini). Ama leo sifanyi biashara miongoni mwenu isipokuwa fulani na fulani.  [Imepokewa na Bukhari na Muslim]


شرح الحديث مع فضيلة الشيخ خالد بن عثمان السبت حفظه الله



 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

 

Visitors Counter

6573118
TodayToday1185
Highest 01-07-2025 : 4073
US
Guests 25

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_682875543552917977293671747481940
title_682875543564618697024641747481940
title_682875543575c19962741111747481940

NISHATI ZA OFISI

title_682875544287220935934171747481940
title_68287554429f810253870511747481940
title_6828755442b7213436223311747481940 Add content here

HUDUMA MPYA

: 8 + 7 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com