BUSTANI YA WATU WEMA


1463655589


{وقال تعالى : {فَمَاذَا بَعْدَ الْحَقِّ إِلَّا الضَّلَالُ

{وقال تعالى : {مَّا فَرَّطْنَا فِي الْكِتَابِ مِن شَيْءٍ

{وقال تعالى : {فَإِن تَنَازَعْتُمْ فِي شَيْءٍ فَرُدُّوهُ إِلَى اللَّهِ وَالرَّسُولِ

{وقال تعالى : {وَأَنَّ هَٰذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ ۖ وَلَا تَتَّبِعُوا السُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَن سَبِيلِهِ

{وقال تعالى : {قُلْ إِن كُنتُمْ تُحِبُّونَ اللَّهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللَّهُ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ

والآيات في الباب كثيرة معلومة


Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

[Na kipo kitu gani baada ya haki, isipokuwa upotovu tu?]       [Suurat Yunus:32]

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

[Hatukupuuza Kitabuni kitu chochote]       [Suurat An'aam:38]

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

[Na mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume]      [Surat An-Nisaai:59]

Na amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

[Na kwa hakika hii ndiyo Njia yangu Iliyo Nyooka. Basi ifuateni, wala msifuate njia nyingine, zikakutengeni na Njia yake.]       [Suurat An'aam:153]

Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

[Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Mwenyezi Mungu basi nifuateni mimi, Mwenyezi Mungu atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu]     [Suurat Al 'Imran:31]

Na Aya katika Mlango huu ni nyingi zenye kujulikana.


شرح مقدمة الباب مع فضيلة الشيخ خالد بن عثمان السبت حفظه الله



 
comments