Menu

SHIRKI KUBWA


shirki kumbwa


Shirki kubwa ni kuamini kwamba mtu au kitu kama vile: Jiwe, mti, nyota, jua, mwezi, mtume, jini, mtu mtakatifu (Saint) au malaika wana uwezo unaofanana na Mwenyezi Mungu kama vile kuruzuku, kutibu, au kulinda na kwamba kinastahiki kuadhimishwa na kuombwa na kuabudiwa.

Au ni kumfanyia Mwenyezi Mungu visawazishi katika Uungu wake au ibada yake au majina yake na sifa zake nzuri.

 

HUKMU YAKE 

Shirki kubwa ndilo dhambi kubwa sana, humtoa mtu katika Wisilamu na damu yake huwa halali kuichukua pamoja na mali yake. Amesema Mtume :

 

 أمرت أن أقاتل الناس حتى يشهدوا أن لا إله إلا الله وأن محمد رسول الله، ويقيموا الصلاة، ويؤتوا الزكاة؛ فإذا فعلوا ذلك عصموا مني دماءهم إلا بحق الإسلام، وحسابهم على الله

 

[Nimeamrishwa kuwa niwapige vita watu mpaka washuhudie kwamba hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki illa Mwenyezi Mungu na kwamba Mohammad ni mjumbe wa Mwenyezi Mungu….]

Ni dhambiambayo Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta´ala) haisamehi. Amesema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta´ala):

 

[ إِنَّ اللَّهَ لا يَغْفِرُ أَنْ يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَلِكَ لِمَنْ يَشَاءُ وَمَنْ يُشْرِكْ بِاللَّهِ فَقَدْ افْتَرَى إِثْمًا عَظِيمًا]    [النساء 48]

 

[Hakika Mwenyezi Mungu hasamehi kushirikishwa; na husamehe yasiyokuwa haya kwa amtakae. Na anaemshirikisha Mwenyezi Mungu bila shaka amebuni dhambi kubwa (kabisa).]    [Suratun-Nisaa ya 48]

 

Luqmaan alijaaliwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu kuwa na hekima sana, naye aliifananisha SHIRKI kuwa sawa na DHULMA KUBWA. Kama alivyosema Mwenyezi Mungu Subhanau Wata'ala kwa kauli ya Luqmaan:


[إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ]    [ لقمان : 13]

 

[Hakika shirki ni dhulma kubwa.]

Pia shirki humsababishia mja kuharamishiwa Pepo kwa uthibitisho wa Qurani tukufu. Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:


[ إِنَّهُ مَنْ يُشْرِكْ بِاللَّهِ فَقَدْ حَرَّمَ اللَّهُ عَلَيْهِ الْجَنَّةَ وَمَأْوَاهُ النَّارُ]      [المائدة : 72]

 

[Kwani anaemshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharamishia Pepo, na mahali pake (patakuwa) ni Motoni.]    [Al Maaida:72]


SIKILIZA MADA HII NA SHEIKH SALIM KHATIB



LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6487087
TodayToday193
Highest 12-07-2024 : 5072
US
Guests 45

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_676e53a2bd81c14195762271735283618
title_676e53a2bd9068499708331735283618
title_676e53a2bd9ea14918936671735283618

NISHATI ZA OFISI

title_676e53a2bef5d4821974411735283618
title_676e53a2c968610576995261735283618
title_676e53a2c978c14979965991735283618 Add content here

HUDUMA MPYA

: 5 + 5 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com