Menu

SOMO LA FIQHI


 somo lafiqhi


Suali: Ni yapi masharti ya mtu kulazimika kutoa zaka? 

Jawabu: Masharti ya mtu kulazimika kutoa Zaka ni kama ya fuatayo:
1. Uislamu
Haikubaliwi Zaka kwa kafiri, kwasababu Mwenyezi Mungu U hakubali matendo yake.

2. Kuwa huru (muungwana).
Haikubaliwi kwa mtumwa kutoa Zaka, kwasababu mali yake ni milki ya bwana wake.

3. Kumiliki Nisabu.(kiwangu)

Suali: Ni nini Maana ya Nisaabu:

Jawabu: Maana ya Nisabu.

Ni kiwango maalumu cha mali ambacho kwamba kikifikiwa basi inalazimika Mali hayo kutolewa Zaka.

Masharti ya Nisabu.

1. Iwe Nisabu ni ziada ya mahitaji ya dharura ambayo kwamba mtu hatosheki kwa kuyapata mahitaji hayo, kama chakula, mavazi na makazi, kwasababu Zaka ni wajibu kwa lengo la kuwaliwaza mafukara. Hivyo basi inatakiwa mwenye kutoa hiyo mali asiwe ni mtu muhitaji.

2. Iwe Nisabu inamilikiwa na mtu maalumu umiliki wa kiukamilifu, basi haiwajibiki Zaka kwa mali ambayo haimilikiwi na mtu maalumu, kwa mfano: mali iliyokusanywa kwa lengo la kujenga msikiti, au mali iliyowekwa wakfu kwa maslahi ya ummah, au mali iliyoko kwenye hazina za jumuia za mambo ya kheri.

4. Mali kupitiwa na Mwaka
Mwaka
Ni mwaka wa kiislamu) uliyokamilika.

Na hii ni kwamba ipite miezi kumi na mbili ya kalenda ya mtizamo wa mwezi hali ya kuwa Nisabu iko kwenye miliki ya mwenye mali. Na sharti hili ni peke yake kwa pesa (dhahabu na fedha), na mapato ya biashara, na wanyama wa mifugo. Ama mazao ya kilimo na matunda, na madini, hazina iliyozikwa ardhini sio sharti kwa vitu hivi kupitiwa na mwaka.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7887144
TodayToday277
Highest 05-20-2026 : 12580
US
Guests 33

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6a3ba223067b020684897311782293027
title_6a3ba223067ff1392269521782293027
title_6a3ba2230683410835681641782293027

NISHATI ZA OFISI

title_6a3ba22306dc1396652361782293027
title_6a3ba22306e0e995178591782293027
title_6a3ba22306e593131666661782293027 Add content here

HUDUMA MPYA

: 6 + 3 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com