Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


1. Kuleta nia kwa sauti wakati wa kutawadha.

2. Kutumia maji kwa kupita kiasi.

3. Kuzidisha maosho matatu katika kutawadha, kwa riwaya iliyopokewa kuwa mbedui alikuja kwa Mtume kumuuliza juu ya kutawadha, akamuonesha udhu mara tatutatu kisha akasema:

 

هَكَذَا الْوُضُوءُ، فَمَنْ زَادَ عَلَى هَذَا فَقَدْ أَسَاءَ وَتَعَدَّى وَظَلَمَ]      رواه أبوداود والنسائي وأحمد]

 

[Kutawadha ni namna hii. Na mwenye kuzidisha hapo amekosea, amepita mpaka na amedhulumu]  [Imepokewa na Abu Daud na Annasai na Ahmad.]

Lakini inafaa kuongeza zaidi ya maosho matatu iwapo atakuwa hakukisafisha kiungo kwa maosho matatu, kama mtu aliyeingiwa na mafuta au kitu kingine mkononi.

4. Kutoeneza maji katika kutawadha, kwa riwaya iliyopokewa kuwa mtu alitawadha, akaacha paku kadiri ya ukucha kwenye nyayo, Mtume akaliona na aksema: [Rudi utawadhe kwa uzuri]   [ Imepokewa na Muslim.] akarudi kisha akaswali.

Na inaingia kwenye kukosa kueneza maji ya udhu:

a- kutoosha vifundo viwili vya miguu

b- kutoosha visukusuku kwa sababu ya wembamba wa mikono ya kanzu.

c- kutoosha weupe ulioko baina ya masikio na ndevu.

d- Kutoosha kitanga cha mkono wa kushoto pamoja na mkono wa kushoto.

e- mwenye kutawadha naye una mapaku ya mafuta.

f- kutawadha kwa mwanamke na juu ya vidole vyake pana pambo lenye kuzuia maji kufika kwenye ngozi.

g- kutofikisha maji kwenye vidole vya miguu iwapo maji hayapiti baina ya vdole.

5. Kupangusa shingo:

Si miongoni mwa matendo ya kutawadha,

6. kuleta dhikiri ambazo hazikuja katika Sheria, mfano:

a- kuomba dua maalumu katika kuosha kila kiungo.

b- kumwambia “zamzam” mwenye kutawadha.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7668187
TodayToday7950
Highest 04-18-2026 : 16767
US
Guests 262

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_69f17e49b26701934072401777434185
title_69f17e49b26d316161276971777434185
title_69f17e49b273018682463301777434185

NISHATI ZA OFISI

title_69f17e49b2ed78456319951777434185
title_69f17e49b2f366916521811777434185
title_69f17e49b2f8720645839971777434185 Add content here

HUDUMA MPYA

: 3 + 6 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com