Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


Tunakusudia kusema kwa istilahi (wenye udhuru) wale watu ambao ambao wana maradhi yanayowafanya wasiweze kuuhifadhi udhu wao kama wanavyoweza watu wengine katika hali ya kawaida.

Hawa ni pamoja na mtu mwenye maradhi ya mchuchuro wa mkojo, hawezi kuuzuia mkojo, saa zote hutokwa na mkojo au anatokwa na upepo (ushuzi) mara kwa mara.

Au mwanamke aliyepatwa na maradhi ya kutokwa na damu ya mbobo/ugonjwa, hii ni damu itokayo kwa wingi katika wakati usiokuwa wa damu ya ada ya kila mwezi (hedhi).

Hukumu ya udhu wa watu hawa ni kwamba wanatakiwa watawadhe kila unapoingia wakati wa kila swala, wasitawadhe kabla ya kuingia wakati kwa kuwa wanatakiwa kufululiza baina ya udhu na swala.

Hii ni kwa sababu kisheria hawana udhu kwani wana hadathi ya kudumu na udhu wao ni wa ruhusa maalum waliyopewa na sheria ili waweze kuyatekeleza yale yote yasiyotekelezeka bila ya udhu, kama vile swala, tawafu na kadhalika.

Wataswali kwa udhu huo swala wazitakazo za suna au za fardhi.

Udhu wa watu hawa utabatilika na kutenguka mara tu unapoingia wakati wa swala nyingine. Akitaka kuswali basi itamlazimu kutawadha tena.

Haya yote yanaonyesha wepesi wa sheria ya Kiislamu ambayo imejengwa juu ya misingi ya wepesi na kuondosha uzito na ugumu. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu :

 

 وَمَا جَعَلَ عَلَيْكُمْ فِي الدِّينِ مِنْ حَرَجٍ ۚ مِلَّةَ أَبِيكُمْ إِبْرَاهِيمَ}   الحج:22}

 

[Wala hakuweka juu yenu mambo mazito katika Dini. Nayo ni mila ya baba yenu Ibrahim.]   [22:78].


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6668134
TodayToday822
Highest 06-05-2025 : 6758
US
Guests 16

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6866b1be3fc0a10142221441751560638
title_6866b1be3fcf64650867111751560638
title_6866b1be3fde45629228251751560638

NISHATI ZA OFISI

title_6866b1be413a512608121751751560638
title_6866b1be4148c9038304691751560638
title_6866b1be4157a20644491961751560638 Add content here

HUDUMA MPYA

: 7 + 3 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com