Menu

SOMO LA FIQHI


 somo lafiqhi


Suali: Ni nini Maana ya Twahara ki Lugha na Kisheria ?

Jawabu: Utwahara kilugha
Kujisafisha na kujitakasa na uchafu

Utwahara kisheria
Utwahara kutokana na Kujitwahirisha na najisi

 

VIGAWANYO VYA TWAHARA

 

Suali: Twahara inagawanyika sehemu ngapi?

Jawabu: Twahara inagawanyika sehemu mbili:

1. UTWAHARA WA NDANI

Nao ni kuusafisha moyo na ushirikina na maasia na kila chenye kuutia doa. Haiwezekani kuhakikishika utwahara iwapo kutakuwa na uchafu wa ushirikina ndani ya moyo, kama ilivyo katika maana ya maneno ya Mwenyezi Mungu:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْمُشْرِكُونَ نَجَسٌ فَلَا يَقْرَبُوا الْمَسْجِدَ الْحَرَامَ بَعْدَ عَامِهِمْ هَٰذَا ۚ وَإِنْ خِفْتُمْ عَيْلَةً فَسَوْفَ يُغْنِيكُمُ اللَّهُ مِن فَضْلِهِ إِن شَاءَ ۚ إِنَّ اللَّهَ عَلِيمٌ حَكِيمٌ   التوبة:28

 

[Enyi Mlioamini! Hakika washirikina ni najisi, basi na wasiukaribie Msikiti wa Haram (Msikiti wa Makka) baada ya mwaka wao huu. Na mkiwa mnaogopa umasikini, basi Mwenyezi Mungu Atawakwasisha nyinyi kwa fadhla Zake. Hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi Mwenye hekima} [8: 28]

Na Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema:

 

المؤمن لا ينجس.]    رواه البخاري]

 

[Muumini hanajisiki.]  [Imepokewa na Bukhari na Muslim]

 

2.UTWAHARA WA NJE

Nao ni utwahara wa mwili kutokana na hadathi na najisi.

Na inagawanyika vigawanyiko viwili:

1.Utwahara kutokana na hadathi (hali ya kutokuwa na udhu na kuwa na janaba)

Hadathi ni kile kinachotukia katika mwili kikamzuia Muislamu kufanya ibada ambazo zinahitaji utwahara, kama kuswali, kutufu kwenye Alkaba na zinginezo. Na inagawanyika vigawanyo viwili:

2. Kujitwahirisha na Najisi:

Nao ni kuiyondoa najisi mwilini na nguoni na sehemu ya kufanya ibada, Na kuondoa najisi ni lazima kwa neno la Mwenyezi Mungu Aliye tukuka:

 

وَثِيَابَكَ فَطَهِّرْ}     المدثر:4}

[Na nguo zako zitwahirishe]  [74: 4]

Na neno lake Mtume ﷺ:

 

قوله صلى الله عليه وسلم : إذا جاء أحدكم إلى المسجد فلينظر فإن رأى في نعليه قذرا أو أذى فليمسحه وليصل فيهما . رواه أبو داود

 

[Mmoja wenu akija msikitini na atazame, akiona uchafu au kitu cha kuudhi kwenye viatu vyake basi na avipanguse kisha aswali navyo].  [Imepokewa na Abuu Daud].


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

7669231
TodayToday896
Highest 04-18-2026 : 16767
US
Guests 210

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_69f19c137ff757355491571777441811
title_69f19c137ffdb11710240691777441811
title_69f19c138003d12443154741777441811

NISHATI ZA OFISI

title_69f19c1380b6b9169027361777441811
title_69f19c1380bcf13697568211777441811
title_69f19c1380c2c20399609701777441811 Add content here

HUDUMA MPYA

: 2 + 3 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com