SOMO LA FIQHI
Kwanini ukaitwa usiku wa cheo (usiku waheshima)?
Wanachuoni wameeleze sababu ya kuitwa usiku huu wa Laylayul na miongoni mwa sababu walizozitaja ni haya yafuatayo
1. Kumesemwa: Ni kwasababu ya kuutukuza, kama ilivyo katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:
وَمَا قَدَرُوا اللَّهَ حَقَّ قَدْرِهِ} الأنعام:91}
[Na (Mayahudi ) hawakumhishimu Mwenyezi Mungu kama inavyotakiwa kumhishimu] [Al-An-a’m – Aya 91].
Na maana yake: Ni kwamba huu usiku ni wenye hishima; kwa kuteremshwa Qur’ani ndani yake na kupatika na kushuka malaika, na ni usiku wa baraka na rehema na msamaha kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
2. Inasemekana: Al-qadr kwa maana ya kubanika kwa kuwa ndogo sana, kama kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu:
وَمَن قُدِرَ عَلَيْهِ رِزْقُهُ فَلْيُنفِقْ مِمَّا آتَاهُ اللَّهُ} الطلاق:7}
[Na yule ambaye amepungukiwa riziki yake (riziki yake imebanika kwa kuwa ndogo sana), atoe katika kile alichopewa na Mwenyezi Mungu] [At-twalaq – Aya 7].
Na maana ya kubanika kwa kuwa ndogo sana: Ni kule kufichika katika elimu za watu kutambua hasa usiku huo ni usiku wa tarehe ngapi.
3. Na inasemekana: Al-qadr kumaanisha makadirio, kwa maana: katika usiku huu ndiyo kunakadiriwa hukumu za mwaka ulioko; kwa kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu:
إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةٍ مُّبَارَكَةٍ ۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ فِيهَا يُفْرَقُ كُلُّ أَمْرٍ حَكِيمٍ} الدخان 3-4}
[Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,] [Ad-Dukhan – Aya 3-4].
Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.